Amosi 4:1-13

  • Ujumbe dhidi ya ng’ombe wa Bashani (1-3)

  • Yehova adhihaki ibada ya uwongo ya Waisraeli (4, 5)

  • Waisraeli wakataa nidhamu (6-13)

    • “Jitayarishe kukutana na Mungu wako” (12)

    • ‘Mungu humwambia mwanadamu mawazo Yake’ (13)

4  “Sikieni neno hili, enyi ng’ombe wa Bashani,Mlio kwenye mlima wa Samaria,+Ninyi wanawake mnaowalaghai watu wa hali ya chini+ na kuwakandamiza maskini,Mnaowaambia waume zenu,* ‘Tuleteeni kinywaji!’   Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameapa kwa utakatifu wake,‘“Tazameni! Siku zinakuja wakati ambapo atawainua juu kwa kulabu za mchinjaji wa wanyamaNa wale watakaobaki kati yenu kwa ndoano za samaki.   Kila mmoja wenu atatoka nje moja kwa moja kupitia sehemu zilizobomolewa ukutani;Nanyi mtatupwa kule Harmoni,” asema Yehova.’   ‘Njooni Betheli mtende dhambi,*+Njooni Gilgali mzidi kutenda dhambi!+ Leteni dhabihu zenu+ asubuhi,Na sehemu zenu za kumi+ katika siku ya tatu.   Teketezeni dhabihu ya shukrani ya mikate iliyotiwa chachu;+Tangazeni kwa sauti matoleo yenu ya hiari! Kwa maana hivyo ndivyo mnavyopenda kufanya, enyi watu wa Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.   ‘Lakini mimi niliyafanya meno yenu yawe safi bila chakula* katika majiji yenu yoteNikasababisha mkose mikate katika nyumba zenu zote;+Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.   ‘Pia niliwanyima mvua miezi mitatu kabla ya mavuno;+Nilileta mvua katika jiji moja lakini sikuileta katika jiji lingine. Shamba moja lilipata mvua,Lakini shamba lingine lilikauka kwa sababu halikupata mvua.   Watu wa majiji mawili au matatu walipepesuka kwenda kwenye jiji moja kunywa maji,+Nao hawakutosheka;Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova.   ‘Niliwapiga kwa joto linalounguza na kuvu.+ Mlizidisha bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu,Lakini nzige walitafuna mitini yenu na mizeituni yenu;+Na bado hamkunirudia,’+ asema Yehova. 10  ‘Niliwaletea ugonjwa hatari kama ule wa* Misri.+ Niliwaua vijana wenu wa kiume+ kwa upanga na kuwateka farasi wenu.+ Nilifanya uvundo wa kambi zenu upande katika mianzi ya pua zenu;+Lakini hamkunirudia,’ asema Yehova. 11  ‘NiliwaangamizaKama Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora.+ Nanyi mlikuwa kama gogo lililochomolewa haraka motoni;Lakini hamkunirudia,’+ asema Yehova. 12  Basi hivyo ndivyo nitakavyokutendea, Ee Israeli. Kwa kuwa nitakutendea hivyo,Jitayarishe kukutana na Mungu wako, Ee Israeli. 13  Kwa maana tazama! yeye Ndiye aliyeumba milima+ na kuumba upepo;+Humwambia mwanadamu mawazo Yake,Hubadili mapambazuko kuwa giza,+Naye hukanyaga vilele vya dunia;+Yehova Mungu wa majeshi ndilo jina lake.”

Maelezo ya Chini

Au “mabwana wenu wakubwa.”
Au “mfanye uasi.”
Au “sikuwapa chakula chochote.”
Au “tauni kama ile ya.”