Amosi 5:1-27

  • Waisraeli ni kama bikira aliyeanguka (1-3)

  • Mtafuteni Yehova, mwendelee kuishi (4-17)

    • Chukieni maovu, pendeni mema (15)

  • Siku ya Yehova itakuwa siku ya giza (18-27)

    • Dhabihu za Waisraeli zakataliwa (22)

5  “Sikieni neno hili ninalosema dhidi yenu kama wimbo wa huzuni,* Ee nyumba ya Israeli:   ‘Bikira, Israeli, ameanguka;Hawezi kuinuka tena. Ameachwa peke yake katika ardhi yake mwenyewe;Hakuna yeyote wa kumwinua.’  “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Jiji linaloenda vitani likiwa na watu elfu moja litabaki na watu mia moja;Na lile linaloenda vitani na watu mia moja litabaki na watu kumi, hili linahusu nyumba ya Israeli.’+  “Kwa maana Yehova anaiambia hivi nyumba ya Israeli: ‘Nitafuteni mimi mwendelee kuishi.+   Msitafute Betheli,+Msiende Gilgali+ wala msivuke kwenda Beer-sheba,+Kwa maana Gilgali hakika litapelekwa uhamishoni,+Na Betheli litaangamizwa.*   Mtafuteni Yehova, mwendelee kuishi,+Ili asilipuke kama moto kwenye nyumba ya Yosefu,Na kuteketeza kabisa Betheli, hivi kwamba hakuna mtu atakayeweza kuuzima moto huo.   Mnabadili haki kuwa pakanga,*Nanyi mnautupa uadilifu ardhini.+   Yule aliyeumba kundi la nyota la Kima* na kundi la nyota la Kesili,*+Yule anayebadili kivuli kizito kuwa asubuhi,Yule anayefanya mchana uwe na giza kama usiku,+Yule anayeyaita maji ya bahariIli ayamwage kwenye nchi kavu+—Yehova ndilo jina lake.   Atasababisha maangamizi yawajie kwa ghafla wenye nguvu,Na kuharibu ngome. 10  Wanawachukia wale wanaotoa karipio kwenye lango la jiji,Na kuwachukia sana watu wanaosema ukweli.+ 11  Kwa sababu mnamdai maskini kodi ya* shambaNanyi mnachukua nafaka yake kama ushuru,+Hamtaendelea kuishi katika nyumba mlizojenga kwa mawe yaliyochongwa+Wala hamtakunywa divai kutoka katika mashamba bora ya mizabibu mliyopanda.+ 12  Kwa maana ninajua jinsi maasi yenu* yalivyo mengiNa jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa—Mnawanyanyasa waadilifu,Mnapokea rushwa,*Nanyi mnawanyima maskini haki zao kwenye lango la jiji.+ 13  Kwa hiyo, wale walio na ufahamu watanyamaza kimya wakati huo,Kwa sababu utakuwa wakati wa msiba.+ 14  Tafuteni yaliyo mema, na wala si maovu,+Ili mwendelee kuishi.+ Ndipo huenda Yehova Mungu wa majeshi atakuwa pamoja nanyi,Kama mnavyosema yuko pamoja nanyi.+ 15  Chukieni maovu, pendeni yaliyo mema,+Acheni haki itawale kwenye lango la jiji.+ Huenda Yehova Mungu wa majeshiAtawaonyesha kibali wazao waliobaki wa Yosefu.’+ 16  “Kwa hiyo Yehova Mungu wa majeshi, Yehova, anasema hivi: ‘Watu watalia kwa sauti katika viwanja vyote vya jiji,Katika barabara zote watasema, “Ole! Ole!” Watawaita wakulima waombolezeNa waombolezaji wa kulipwa walie kwa sauti.’ 17  ‘Kutakuwa na kilio katika kila shamba la mizabibu;+Kwa maana nitapita katikati yenu,’ asema Yehova. 18  ‘Ole wao wanaoitamani siku ya Yehova!+ Basi, siku ya Yehova itamaanisha nini kwenu?+ Itakuwa giza, wala si nuru.+ 19  Itakuwa kama mtu anayemkimbia simba, kisha anakutana na dubu,Na anapoingia nyumbani mwake na kuuegemeza mkono wake ukutani, anaumwa na nyoka. 20  Je, siku ya Yehova haitakuwa giza, wala si nuru;Je, haitakuwa na utusitusi, wala si mwangaza? 21  Nazichukia, nazidharau sherehe zenu,+Nami sifurahii harufu tamu ya makusanyiko yenu matakatifu. 22  Hata mkinitolea dhabihu nzima za kuteketezwa na matoleo ya zawadi,Sitazifurahia;+Nami sitapendezwa na dhabihu zenu za ushirika za wanyama waliononeshwa.+ 23  Niondoleeni kelele za nyimbo zenu;Na sitaki kusikia miziki ya vinanda vyenu.+ 24  Acheni haki itiririke kama maji,+Na uadilifu kama kijito kinachotiririka daima. 25  Je, uliniletea dhabihu na matoleo ya zawadiKwa miaka 40 uliyokuwa nyikani, Ee nyumba ya Israeli?+ 26  Sasa mtalazimika kumchukua Sakuthi mfalme wenu na Kaiwani,*Sanamu zenu, nyota ya mungu wenu ambaye mlijitengenezea, 27  Nami nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Damasko,’+ anasema yeye ambaye jina lake ni Yehova Mungu wa majeshi.”+

Maelezo ya Chini

Au “wimbo wa maombolezo.”
Au labda, “litakuwa kitu cha uchawi.”
Au “uchungu.”
Labda ni kundi la nyota la Orioni.
Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.
Au “ushuru wa.”
Au “hongo.”
Au “matendo yenu ya uhalifu.”
Huenda miungu hiyo miwili inarejelea sayari ya Zohali, ambayo iliabudiwa kama mungu.