Amosi 7:1-17

  • Maono yanayoonyesha mwisho wa Israeli unakaribia (1-9)

  • Amosi aambiwa aache kutabiri (10-17)

7  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinionyesha mambo haya: Tazama! Alileta kundi la nzige mimea ya mwisho* ilipokuwa ikianza kuchipuka. Mimea hiyo ilipandwa baada ya nyasi za mfalme kukatwa.  Kundi hilo la nzige lilipomaliza kula mimea nchini, nikasema: “Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, tafadhali samehe!+ Yakobo ataendeleaje kuishi?* Kwa maana yuko dhaifu!”+  Basi Yehova akafikiria upya* jambo hilo.+ Yehova akasema, “Hilo halitatokea.”  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova alinionyesha mambo haya: Tazama! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova aliamuru moto uje kuwaadhibu. Ukateketeza vilindi vikubwa vya maji, na kuteketeza sehemu ya nchi.  Kisha nikasema: “Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, tafadhali lizuie jambo hili lisitendeke.+ Yakobo ataendeleaje kuishi?* Kwa maana yuko dhaifu!”+  Basi Yehova akafikiria upya* jambo hilo.+ Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova akasema, “Hilo pia halitatokea.”  Alinionyesha mambo haya: Tazama! Yehova alikuwa amesimama juu ya ukuta uliojengwa kwa timazi,* na timazi ilikuwa mkononi mwake.  Kisha Yehova akaniuliza: “Unaona nini, Amosi?” Nikamjibu: “Timazi.” Ndipo Yehova akasema: “Tazama naweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli. Sitawasamehe tena.+  Sehemu za juu za Isaka+ zitaachwa ukiwa, na mahali patakatifu pa Waisraeli pataharibiwa kabisa;+ nami nitaishambulia nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”+ 10  Kuhani Amazia wa Betheli+ akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Yeroboamu+ wa Israeli: “Amosi anapanga njama dhidi yako katikati kabisa ya nyumba ya Israeli.+ Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.+ 11  Kwa maana Amosi anasema hivi: ‘Yeroboamu atauawa kwa upanga; na kwa hakika Waisraeli watapelekwa uhamishoni kutoka katika nchi yao.’”+ 12  Kisha Amazia akamwambia Amosi: “Ee mwonaji, nenda, kimbia uende katika nchi ya Yuda, jitafutie mkate wako* huko, nawe unaweza kutoa unabii wako huko.+ 13  Lakini usiendelee kutoa unabii hapa Betheli,+ kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme+ na nyumba ya ufalme.” 14  Ndipo Amosi akamjibu hivi Amazia: “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii; bali nilikuwa mchungaji wa mifugo,+ nami nilitunza mitini ya mikuyu.* 15  Lakini Yehova aliniondoa katika kazi ya kuchunga kundi, kisha Yehova akaniambia, ‘Nenda, toa unabii kwa watu wangu Waisraeli.’+ 16  Basi sasa sikia neno la Yehova: ‘Wewe unasema: “Usitoe unabii dhidi ya Israeli,+ na usihubiri+ dhidi ya nyumba ya Isaka.” 17  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Mke wako atakuwa kahaba jijini, na wana wako na mabinti wako watauawa kwa upanga. Ardhi yako itagawanywa kwa wengine kwa kamba ya kupimia, na wewe mwenyewe utafia katika nchi isiyo safi; na kwa hakika Waisraeli watapelekwa uhamishoni kutoka katika nchi yao.”’”+

Maelezo ya Chini

Yaani, mwezi wa Januari na Februari.
Tnn., “atainukaje?”
Au “akaghairi kuhusu.”
Tnn., “atainukaje?”
Au “akaghairi kuhusu.”
Au “chubwi; bildi.”
Au “kula mkate.”
Au “nilichanja tini za mikuyu.”