Ayubu 27:1-23

  • Ayubu aazimia kuendelea kuwa mtimilifu (1-23)

    • “Sitaukana utimilifu wangu” (5)

    • Anayemkataa Mungu hana tumaini (8)

    • “Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?” (12)

    • Mtu mwovu habaki na chochote (13-23)

27  Ayubu akaendelea kuzungumza:*   “Kwa hakika kama Mungu anavyoishi, ambaye ameninyima haki,+Kama Mweza-Yote anavyoishi, ambaye amenitia uchungu,+   Maadamu pumzi imo ndani yanguNa roho ya Mungu imo ndani ya mianzi ya pua yangu,+   Midomo yangu haitasema uovu;Wala ulimi wangu hautasema udanganyifu!   Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa waadilifu! Mpaka nitakapokufa, sitaukana* utimilifu wangu!+   Nitadumisha uadilifu wangu, nami sitauacha kamwe;+Moyo wangu hautanihukumu* maadamu ninaishi.*   Adui yangu na awe kama watu waovu,Wale wanaonishambulia na wawe kama watu wasio waadilifu.   Kwa maana mtu anayemkataa Mungu* ana tumaini gani anapoangamizwa,+Mungu anapoondoa uhai wake?*   Je, Mungu atasikia kilio chakeTaabu itakapomjia?+ 10  Au, je, atapendezwa na Mweza-Yote? Je, atamlilia Mungu nyakati zote? 11  Nitawafundisha kuhusu nguvu za* Mungu;Sitaficha jambo lolote kumhusu Mweza-Yote. 12  Tazama! Ikiwa ninyi nyote mmeona maono,Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote? 13  Hilo ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu,+Urithi ambao wakandamizaji hupokea kutoka kwa Mweza-Yote. 14  Wanawe wakiwa wengi, watauawa kwa upanga,+Na wazao wake hawatakuwa na chakula cha kutosha. 15  Pigo litawazika wazao wake watakaobaki,Na wajane wao hawatawalilia. 16  Hata akikusanya fedha kama mavumbiNa kuhifadhi mavazi bora kama udongo wa mfinyanzi, 17  Hata akiyakusanya,Mwadilifu ndiye atakayeyavaa,+Na wanyoofu watagawana fedha zake. 18  Nyumba anayojenga ni dhaifu kama kifuko cha nondo,*Kama kibanda+ kilichojengwa na mlinzi. 19  Ataenda kitandani akiwa tajiri lakini hatakusanya chochote;Atakapofungua macho yake, hakutakuwa na chochote. 20  Hofu humkumba kama mafuriko;Dhoruba humnyakua wakati wa usiku.+ 21  Upepo wa mashariki utampeperusha, naye atatoweka;Utamfagilia mbali kutoka mahali pake.+ 22  Utampiga bila huruma+Huku akijaribu bila mafanikio kuzikimbia nguvu zake.+ 23  Upepo huo humpigia makofiNa kumpigia mluzi+ kutoka mahali ulipo.*

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoa methali.”
Au “sitajiondolea; nitadumisha.”
Au “hautanidhihaki.”
Au “siku yoyote maishani mwangu.”
Au “mwasi imani.”
Au “nafsi yake.”
Au labda, “kwa mkono wa.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au labda, “Wanampigia makofi na kumpigia mluzi kutoka mahali pao.”