Ezekieli 38:1-23

  • Gogu kushambulia Israeli (1-16)

  • Hasira ya Yehova dhidi ya Gogu (17-23)

    • ‘Mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova’ (23)

38  Neno la Yehova likanijia tena likisema:  “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako dhidi ya Gogu wa nchi ya Magogu,+ kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali,+ na utabiri dhidi yake.+  Sema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama, niko dhidi yako, ewe Gogu, kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali.  Nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako+ na kukutoa pamoja na jeshi lako lote,+ farasi na wapanda farasi, wote wakiwa wamevaa mavazi ya kifahari, kusanyiko kubwa sana lenye ngao kubwa na ngao ndogo,* wote wakiwa na mapanga;  Uajemi, Ethiopia, na Putu+ wako pamoja nao, wote wakiwa na ngao ndogo na kofia;  Gomeri na wanajeshi wake wote, watu wa nyumba ya Togarma+ kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, pamoja na wanajeshi wake wote—mataifa mengi yako pamoja nawe.+  “‘“Uwe tayari, ujitayarishe, wewe pamoja na majeshi yako yote yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe utakuwa kamanda* wao.  “‘“Utakaziwa fikira* baada ya siku nyingi. Katika miaka ya mwisho utaishambulia nchi ambayo watu wake wamerudishwa kutoka kwenye uharibifu wa upanga, waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa mengi, na kuletwa kwenye milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imebaki ukiwa. Wakaaji wa nchi hii walirudishwa kutoka katika mataifa, na wote wanakaa kwa usalama.+  Utawashambulia kama dhoruba nawe utaifunika nchi kama mawingu, wewe na wanajeshi wako wote na mataifa mengi pamoja nawe.”’ 10  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku hiyo mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utapanga njama ya uovu. 11  Utasema: “Nitaivamia nchi yenye vijiji visivyo na ulinzi.*+ Nitawashambulia wale wanaokaa kwa usalama, bila usumbufu, wote wanaoishi katika vijiji visivyolindwa na ukuta, makomeo, au malango.” 12  Ili kupora na kuchukua nyara nyingi, ili kushambulia maeneo yaliyoharibiwa ambayo sasa yanakaliwa na watu+ waliokusanywa kutoka katika mataifa,+ ambao wanajikusanyia utajiri na mali,+ wale wanaoishi katikati ya dunia. 13  “‘Sheba+ na Dedani,+ wafanyabiashara wa Tarshishi+ na mashujaa* wake wote watakuuliza: “Je, unavamia ili upore na kupata nyara nyingi? Je, umekusanya majeshi yako ili kubeba fedha na dhahabu, kuchukua utajiri na mali, ili kuteka nyara nyingi sana?”’ 14  “Basi tabiri, mwana wa binadamu, nawe umwambie Gogu, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Siku ambayo watu wangu Waisraeli watakapokuwa wakiishi kwa usalama, je, hutajua jambo hilo?+ 15  Utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini,+ wewe pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, jeshi kubwa sana.+ 16  Kama mawingu yanayoifunika nchi, utawashambulia watu wangu Waisraeli. Katika kipindi cha mwisho cha zile siku, nitakuleta uishambulie nchi yangu+ ili mataifa yanijue nitakapojitakasa mwenyewe kupitia wewe mbele ya macho yao, ewe Gogu.”’+ 17  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Je, wewe si yuleyule niliyesema kumhusu katika siku za zamani kupitia watumishi wangu manabii wa Israeli, waliotabiri kwa miaka mingi kwamba utaletwa ili kuwashambulia?’ 18  “‘Siku hiyo, siku ambayo Gogu ataishambulia nchi ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ghadhabu yangu kali itawaka.+ 19  Kwa bidii yangu, kwa moto wa ghadhabu yangu, nitazungumza; na siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la ardhi katika nchi ya Israeli. 20  Kwa sababu yangu, samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa mwituni, wanyama wote wanaotambaa juu ya nchi, na wanadamu wote walio duniani watatetemeka, nayo milima itaangushwa chini,+ na miamba itaanguka, na kila ukuta utaporomoka.’ 21  “‘Nitauita upanga umshambulie kwenye milima yangu yote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Upanga wa kila mtu utamshambulia ndugu yake mwenyewe.+ 22  Nitamletea hukumu yangu* kwa ugonjwa hatari+ na kwa umwagaji wa damu; nami nitaleta dhidi yake mvua kubwa ya mafuriko na mawe ya mvua+ na moto+ na kiberiti+ na dhidi ya wanajeshi wake na dhidi ya mataifa mengi yaliyo pamoja naye.+ 23  Nami hakika nitajitukuza na kujitakasa na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

Maelezo ya Chini

Au “mkuu wa wakuu.”
Au “mkuu wa wakuu.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Tnn., “mlinzi.”
Au “Utaitwa.”
Au “eneo lililo wazi la mashambani.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “Nitamhukumu.”