Ezra 2:1-70

  • Orodha ya watu waliorudi kutoka uhamishoni (1-67)

    • Watumishi wa hekaluni (43-54)

    • Wana wa watumishi wa Sulemani (55-57)

  • Matoleo ya hiari kwa ajili ya hekalu (68-70)

2  Hawa ndio watu wa mkoa,* baadhi ya mateka waliopanda kutoka uhamishoni,+ ambao Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni Babiloni+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake,+  wale waliokuja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigvai, Rehumu, na Baana. Idadi ya wanaume Waisraeli ilitia ndani:+  wana wa Paroshi, 2,172;  wana wa Shefatia, 372;  wana wa Ara,+ 775;  wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu, 2,812;  wana wa Elamu,+ 1,254;  wana wa Zatu,+ 945;  wana wa Zakai, 760; 10  wana wa Bani, 642; 11  wana wa Bebai, 623; 12  wana wa Azgadi, 1,222; 13  wana wa Adonikamu, 666; 14  wana wa Bigvai, 2,056; 15  wana wa Adini, 454; 16  wana wa Ateri, wa Hezekia, 98; 17  wana wa Besai, 323; 18  wana wa Yora, 112; 19  wana wa Hashumu,+ 223; 20  wana wa Gibari, 95; 21  wana wa Bethlehemu, 123; 22  wanaume wa Netofa, 56; 23  wanaume wa Anathothi,+ 128; 24  wana wa Azmavethi, 42; 25  wana wa Kiriath-yearimu, Kefira na Beerothi, 743; 26  wana wa Rama+ na Geba,+ 621; 27  wanaume wa Mikmasi, 122; 28  wanaume wa Betheli na Ai,+ 223; 29  wana wa Nebo,+ 52; 30  wana wa Magbishi, 156; 31  wana wa Elamu mwingine, 1,254; 32  wana wa Harimu, 320; 33  wana wa Lodi, Hadidi na Ono, 725; 34  wana wa Yeriko, 345; 35  wana wa Senaa, 3,630. 36  Makuhani:+ wana wa Yedaya+ wa nyumba ya Yeshua,+ 973; 37  wana wa Imeri,+ 1,052; 38  wana wa Pashuri,+ 1,247; 39  wana wa Harimu,+ 1,017. 40  Walawi:+ wana wa Yeshua na Kadmieli,+ wa wana wa Hodavia, 74. 41  Waimbaji:+ wana wa Asafu,+ 128. 42  Wana wa walinzi wa malango:+ wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni,+ wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai, wote pamoja walikuwa 139. 43  Watumishi wa hekaluni:*+ wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi, 44  wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni, 45  wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu, 46  wana wa Hagabu, wana wa Salmai, wana wa Hanani, 47  wana wa Gideli, wana wa Gahari, wana wa Reaya, 48  wana wa Resini, wana wa Nekoda, wana wa Gazamu, 49  wana wa Uza, wana wa Pasea, wana wa Besai, 50  wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu, 51  wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri, 52  wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha, 53  wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema, 54  wana wa Nezia, wana wa Hatifa. 55  Wana wa watumishi wa Sulemani: wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda,+ 56  wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli, 57  wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Ami. 58  Watumishi wote wa hekaluni* na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392. 59  Na hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kama ukoo wao* na asili yao ilikuwa ya Waisraeli:+ 60  wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, 652. 61  Na kutoka kwa wana wa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai, aliyemwoa mmoja kati ya mabinti wa Barzilai+ Mgileadi na kuitwa kwa jina lao. 62  Hao walichunguza kumbukumbu zao ili wathibitishe ukoo wao, lakini hawakupata majina ya koo zao, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 63  Gavana* akawaambia kwamba hawangeweza kula vitu vitakatifu kabisa+ mpaka apatikane kuhani ambaye angechunguza Urimu na Thumimu.+ 64  Kutaniko lote lilikuwa na jumla ya watu 42,360,+ 65  mbali na watumwa wao wa kiume na wa kike, ambao walikuwa 7,337; walikuwa pia na waimbaji 200 wa kiume na wa kike. 66  Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, 67  ngamia 435, na punda 6,720. 68  Walipofika kwenye nyumba ya Yehova kule Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa koo* wakatoa matoleo ya hiari+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli, ili kuijenga upya* mahali ilipokuwa.+ 69  Kulingana na uwezo wao walitoa mchango kwa ajili ya hazina ya kazi, drakma 61,000 za dhahabu,* na mina 5,000 za fedha,*+ na kanzu 100 za makuhani. 70  Na makuhani, Walawi, baadhi ya watu, waimbaji, walinzi wa malango, na watumishi wa hekaluni,* wakaanza kuishi katika majiji yao. Na Waisraeli wengine wote* wakaanza kuishi katika majiji yao.+

Maelezo ya Chini

Au “wilaya ya utawala.”
Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”
Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “hawakustahili utumishi wa kikuhani kwa sababu hawakuwa safi.”
Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “kuisimamisha.”
Kwa kawaida drakma ilikuwa sawa na dariki ya dhahabu ya Uajemi yenye uzito wa gramu 8.4. Si drakma ya Maandiko ya Kigiriki. Angalia Nyongeza B14.
Mina inayotajwa katika Maandiko ya Kiebrania ilikuwa na uzito wa gramu 570. Angalia Nyongeza B14.
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Tnn., “Waisraeli wote.”