Hesabu 2:1-34
-
Kambi yapangwa katika makundi ya makabila matatu-matatu (1-34)
2 Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni:
2 “Waisraeli wanapaswa kupiga kambi mahali ambapo kundi lao la makabila matatu+ limegawiwa, kila mtu karibu na alama ya ukoo wake.* Wanapaswa kupiga kambi kuelekeana na hema la mkutano, kuzunguka pande zake zote.
3 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Yuda litapiga kambi upande wa mashariki, upande wa mapambazuko ya jua, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu.
4 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 74,600.+
5 Kabila la Isakari litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari.
6 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 54,400.+
7 Kisha kabila la Zabuloni; mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni.
8 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 57,400.+
9 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Yuda ni 186,400. Wanapaswa kuwa wa kwanza kuondoka.+
10 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni+ litapiga kambi upande wa kusini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri.
11 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 46,500.+
12 Kabila la Simeoni litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai.
13 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 59,300.+
14 Kisha kabila la Gadi; mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli.
15 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 45,650.+
16 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Rubeni ni 151,450, nao wanapaswa kuwa wa pili kuondoka.+
17 “Hema la mkutano linapohamishwa,+ kambi ya Walawi inapaswa kuwa katikati ya kambi nyingine zote.
“Wote wanapaswa kusafiri kwa kufuata utaratibu uleule wanaofuata wanapopiga kambi,+ kila mtu mahali pake, kulingana na makundi yao ya makabila matatu-matatu.
18 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Efraimu litapiga kambi upande wa magharibi, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi.
19 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 40,500.+
20 Kabila la Manase+ litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri.
21 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 32,200.+
22 Kisha kabila la Benjamini; mkuu wa wana wa Benjamini ni Abidani+ mwana wa Gideoni.
23 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 35,400.+
24 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Efraimu ni 108,100, nao wanapaswa kuwa wa tatu kuondoka.+
25 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Dani litapiga kambi upande wa kaskazini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai.
26 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 62,700.+
27 Kabila la Asheri litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani.
28 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 41,500.+
29 Kisha kabila la Naftali; mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani.
30 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 53,400.+
31 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuwa wa mwisho kuondoka,+ kulingana na kundi lao lenye makabila matatu.”
32 Hao ndio Waisraeli walioandikishwa kulingana na koo zao;* watu wote walioandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa 603,550.+
33 Lakini kama Yehova alivyomwamuru Musa, Walawi hawakuandikishwa+ pamoja na Waisraeli wengine.+
34 Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kulingana na makundi yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyokuwa wakiondoka,+ kila mmoja kulingana na familia yake na ukoo wake.*
Maelezo ya Chini
^ Yaani, ukoo wa upande wa baba.
^ Tnn., “majeshi yake.”
^ Tnn., “majeshi yake.”
^ Tnn., “majeshi yake.”
^ Tnn., “majeshi yake.”
^ Yaani, ukoo wa upande wa baba.
^ Yaani, ukoo wa upande wa baba.