Hesabu 2:1-34

  • Kambi yapangwa katika makundi ya makabila matatu-matatu (1-34)

    • Kundi la Yuda upande wa mashariki (3-9)

    • Kundi la Rubeni upande wa kusini (10-16)

    • Kambi ya Lawi yawekwa katikati (17)

    • Kundi la Efraimu upande wa magharibi (18-24)

    • Kundi la Dani upande wa kaskazini (25-31)

    • Jumla ya wanaume walioandikishwa (32-34)

2  Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni:  “Waisraeli wanapaswa kupiga kambi mahali ambapo kundi lao la makabila matatu+ limegawiwa, kila mtu karibu na alama ya ukoo wake.* Wanapaswa kupiga kambi kuelekeana na hema la mkutano, kuzunguka pande zake zote.  “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Yuda litapiga kambi upande wa mashariki, upande wa mapambazuko ya jua, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu.  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 74,600.+  Kabila la Isakari litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari.  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 54,400.+  Kisha kabila la Zabuloni; mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni.  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 57,400.+  “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Yuda ni 186,400. Wanapaswa kuwa wa kwanza kuondoka.+ 10  “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni+ litapiga kambi upande wa kusini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 46,500.+ 12  Kabila la Simeoni litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 59,300.+ 14  Kisha kabila la Gadi; mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 45,650.+ 16  “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Rubeni ni 151,450, nao wanapaswa kuwa wa pili kuondoka.+ 17  “Hema la mkutano linapohamishwa,+ kambi ya Walawi inapaswa kuwa katikati ya kambi nyingine zote. “Wote wanapaswa kusafiri kwa kufuata utaratibu uleule wanaofuata wanapopiga kambi,+ kila mtu mahali pake, kulingana na makundi yao ya makabila matatu-matatu. 18  “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Efraimu litapiga kambi upande wa magharibi, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 40,500.+ 20  Kabila la Manase+ litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 32,200.+ 22  Kisha kabila la Benjamini; mkuu wa wana wa Benjamini ni Abidani+ mwana wa Gideoni. 23  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 35,400.+ 24  “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Efraimu ni 108,100, nao wanapaswa kuwa wa tatu kuondoka.+ 25  “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Dani litapiga kambi upande wa kaskazini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 62,700.+ 27  Kabila la Asheri litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 41,500.+ 29  Kisha kabila la Naftali; mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30  Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 53,400.+ 31  “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuwa wa mwisho kuondoka,+ kulingana na kundi lao lenye makabila matatu.” 32  Hao ndio Waisraeli walioandikishwa kulingana na koo zao;* watu wote walioandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa 603,550.+ 33  Lakini kama Yehova alivyomwamuru Musa, Walawi hawakuandikishwa+ pamoja na Waisraeli wengine.+ 34  Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kulingana na makundi yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyokuwa wakiondoka,+ kila mmoja kulingana na familia yake na ukoo wake.*

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.