Hesabu 25:1-18

  • Waisraeli watenda dhambi na wanawake Wamoabu (1-5)

  • Finehasi achukua hatua (6-18)

25  Waisraeli walipokuwa wakikaa Shitimu,+ watu walianza kufanya uasherati na mabinti wa Moabu.+  Wanawake hao waliwaalika kwenye dhabihu za miungu yao,+ nao watu wakaanza kula na kuinamia miungu yao.+  Kwa hiyo Waisraeli wakashiriki katika kumwabudu* Baali wa Peori,+ na hasira ya Yehova ikawaka dhidi yao.  Yehova akamwambia Musa: “Wachukue viongozi wote wa watu hawa na uwatundike kweupe kabisa wakati wa mchana* mbele za Yehova, ili hasira kali ya Yehova isiendelee kuwaka dhidi ya Waisraeli.”  Kisha Musa akawaambia hivi waamuzi wa Israeli:+ “Kila mmoja wenu awaue watu wake walioshiriki katika kumwabudu* Baali wa Peori.”+  Lakini wakati huo, Mwisraeli fulani akamleta mwanamke Mmidiani+ karibu na ndugu zake Waisraeli huku Musa na Waisraeli wote wakitazama walipokuwa wakilia kwenye mlango wa hema la mkutano.  Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa kuhani Haruni alipoona jambo hilo, aliinuka mara moja kutoka kati ya Waisraeli waliokusanyika, akachukua mkuki.  Kisha akamfuata mwanamume huyo Mwisraeli mpaka hemani, akawachoma mkuki wote wawili, nao ukapenya kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke huyo. Ndipo pigo lililowapata Waisraeli likakomeshwa.+  Watu waliokufa kutokana na pigo hilo walikuwa 24,000.+ 10  Kisha Yehova akamwambia Musa: 11  “Finehasi+ mwana wa Eleazari mwana wa kuhani Haruni amezuia ghadhabu yangu dhidi ya Waisraeli kwa sababu hakuvumilia ushindani wowote dhidi yangu miongoni mwao.+ Kwa hiyo sijawaangamiza Waisraeli licha ya kwamba ninasisitiza watu waniabudu mimi peke yangu.+ 12  Kwa hiyo mwambie, ‘Ninafanya agano langu la amani pamoja naye. 13  Nalo litakuwa agano la ukuhani wa kudumu kwa ajili yake na wazao wake,+ kwa maana hakuvumilia ushindani wowote kumwelekea Mungu wake,+ naye alifanya dhambi ya Waisraeli ifunikwe.’” 14  Sasa, mwanamume huyo Mwisraeli aliyeuawa pamoja na mwanamke Mmidiani aliitwa Zimri mwana wa Salu, mkuu wa ukoo* wa Wasimeoni. 15  Mwanamke Mmidiani aliyeuawa aliitwa Kozbi binti ya Suri;+ Suri alikuwa kiongozi wa koo* za nyumba fulani huko Midiani.+ 16  Baadaye Yehova akamwambia Musa: 17  “Wachokozeni Wamidiani na kuwaangamiza,+ 18  kwa sababu wamekuwa wakiwachokoza kwa hila zao kama ilivyokuwa kule Peori+ na pia kuhusiana na Kozbi binti ya mkuu wa Midiani, dada yao aliyeuawa+ wakati pigo lilipotokea kwa sababu ya mambo yaliyotokea Peori.”+

Maelezo ya Chini

Au “wakashikamana na.”
Au “juani.”
Au “walioshikamana na.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.