Hesabu 4:1-49

  • Utumishi wa Wakohathi (1-20)

  • Utumishi wa Wagershoni (21-28)

  • Utumishi wa Wamerari (29-33)

  • Muhtasari kuhusu idadi ya watu waliohesabiwa (34-49)

4  Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni:  “Mnapaswa kuwahesabu wana wa Kohathi+ miongoni mwa wana wa Lawi, kulingana na familia zao na koo zao,*  wote wenye umri wa miaka 30+ hadi 50+ walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+  “Huu ndio utumishi wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+ Unahusiana na vitu vitakatifu kabisa:  Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wanawe wataingia na kulishusha pazia linaloning’inia mbele ya sanduku la Ushahidi+ na kulifunika kwa pazia hilo.+  Wataweka kifuniko cha ngozi ya sili juu yake na kutandaza juu yake kitambaa cha bluu, halafu wataingiza fito za kubebea+ sanduku hilo.  “Pia watafunika meza ya mikate ya wonyesho+ kwa kitambaa cha bluu, na juu yake wataweka sahani, vikombe, mabakuli, na magudulia ya toleo la kinywaji;+ mikate ya wonyesho ambayo huwa juu ya meza hiyo daima+ inapaswa kubaki juu yake.  Watafunika vitu hivyo kwa kitambaa chekundu na juu yake wataweka kifuniko cha ngozi ya sili na kuingiza fito za kuibeba.+  Kisha watachukua kitambaa cha bluu na kukifunika kinara cha taa+ pamoja na taa zake,+ koleo zake, vyetezo vyake,+ na vyombo vyake vyote vya kuwekea mafuta. 10  Nao wataweka kinara hicho pamoja na vyombo vyake vyote ndani ya ngozi ya sili na kukiweka juu ya ufito wa kubebea. 11  Kisha watatandaza kitambaa cha bluu juu ya madhabahu ya dhahabu+ na kuifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili, halafu wataingiza fito za kuibeba.+ 12  Nao watachukua vyombo vyote+ wanavyotumia kwa ukawaida wanapohudumu mahali patakatifu na kuviweka ndani ya kitambaa cha bluu na kuvifunika kwa kifuniko cha ngozi ya sili, kisha wataviweka juu ya ufito wa kubebea. 13  “Wataondoa majivu* yaliyo kwenye madhabahu+ na kutandaza kitambaa cha sufu cha zambarau juu ya madhabahu hiyo. 14  Kisha wataweka juu yake vyombo vyake vyote wanavyotumia kuhudumu kwenye madhabahu: vyetezo, nyuma,* sepetu, na mabakuli, vyombo vyote vya madhabahu;+ watatandaza juu yake kifuniko cha ngozi ya sili na kuingiza fito za kuibeba.+ 15  “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano. 16  “Eleazari+ mwana wa kuhani Haruni ana jukumu la kusimamia mafuta kwa ajili ya taa,+ uvumba uliotiwa manukato,+ toleo la kawaida la nafaka, na mafuta yanayotumiwa kutia mafuta.+ Ndiye anayesimamia hema lote la ibada na vitu vyote vilivyomo, pamoja na mahali patakatifu na vyombo vyake.” 17  Yehova akaendelea kumwambia Musa na Haruni: 18  “Msiache familia za Wakohathi+ ziangamizwe kutoka miongoni mwa Walawi. 19  Lakini fanyeni jambo hili ili waendelee kuishi nao wasife kwa sababu ya kukaribia vitu vitakatifu kabisa.+ Haruni na wanawe wataingia humo na kumgawia kila mmoja wao kazi yake na vitu anavyopaswa kubeba. 20  Hawapaswi kuingia hemani na kuona vitu vitakatifu hata kwa muda mfupi, la sivyo watakufa.”+ 21  Kisha Yehova akamwambia Musa: 22  “Wana wa Gershoni+ wanapaswa kuhesabiwa kulingana na koo zao* na familia zao. 23  Utawaandikisha wanaume wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 24  Huu ndio utumishi ambao watu wa familia za Wagershoni wamegawiwa kufanya na vitu wanavyopaswa kubeba:+ 25  Watabeba vitambaa vya hema la ibada,+ hema la mkutano, kifuniko chake na kifuniko cha ngozi ya sili kilicho juu yake,+ pazia la mlango wa hema la mkutano,+ 26  mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ unaozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema hilo na vyombo vyake vyote, na vitu vyote vinavyotumiwa katika utumishi wa hema la ibada. Hiyo ndiyo kazi waliyogawiwa. 27  Haruni na wanawe watasimamia utumishi wote wa Wagershoni+ pamoja na vitu wanavyopaswa kubeba; utawapa jukumu la kubeba vitu hivyo vyote. 28  Huo ndio utumishi utakaofanywa na familia za Wagershoni katika hema la mkutano;+ watasimamiwa na Ithamari+ mwana wa kuhani Haruni. 29  “Utawaandikisha wana wa Merari+ kulingana na familia zao na ukoo wao.* 30  Utawaandikisha wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 31  Ni jukumu lao kubeba+ vitu vifuatavyo vinavyohusiana na utumishi wao katika hema la mkutano: viunzi+ vya hema la ibada, fito zake,+ nguzo zake,+ vikalio vyake;+ 32  nguzo+ za ua unaozunguka pande zote, vikalio vyake,+ vigingi vyake vya hema,+ na kamba za hema hilo pamoja na vifaa vyake vyote na utumishi wote unaohusiana na hema la ibada. Utamgawia kila mmoja wao kwa jina vifaa anavyopaswa kubeba. 33  Hivyo ndivyo familia za wana wa Merari+ zitakavyotumikia katika hema la mkutano chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.”+ 34  Kisha Musa na Haruni na wakuu+ wa Israeli wakawaandikisha wana wa Kohathi+ kulingana na familia zao na ukoo wao,* 35  wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+ 36  Wote walioandikishwa kulingana na familia zao walikuwa 2,750.+ 37  Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za Wakohathi, wote walitumikia katika hema la mkutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa.+ 38  Wana wa Gershoni+ waliandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao,* 39  wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano. 40  Wote walioandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao* walikuwa 2,630.+ 41  Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za wana wa Gershoni, wote walitumikia katika hema la mkutano. Musa na Haruni waliwaandikisha kama Yehova alivyoagiza.+ 42  Wana wa Merari waliandikishwa kulingana na familia zao na ukoo wao,* 43  wote wenye umri wa miaka 30 hadi 50 walio katika kikundi kilichogawiwa kutumikia katika hema la mkutano.+ 44  Wote walioandikishwa kulingana na familia zao walikuwa 3,200.+ 45  Hao ndio walioandikishwa kutoka katika familia za wana wa Merari, ambao waliandikishwa na Musa na Haruni kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa.+ 46  Musa na Haruni na wakuu wa Israeli waliwaandikisha Walawi hao wote kulingana na familia zao na koo zao;* 47  walikuwa na umri wa miaka 30 hadi miaka 50, na wote waligawiwa kazi ya kutumikia katika hema la mkutano na kubeba mizigo ya hema hilo.+ 48  Wote walioandikishwa walikuwa 8,580.+ 49  Waliandikishwa kama Yehova alivyoagiza kupitia Musa, kila mmoja wao kulingana na utumishi wake na mzigo aliopaswa kubeba; waliandikishwa kama Yehova alivyomwamuru Musa.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “majivu yenye mafuta,” yaani, majivu yaliyojaa mafuta ya dhabihu.
Wingi wa kifaa kinachoitwa uma.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.