Hosea 1:1-11

  • Mke wa Hosea na watoto anaozaa (1-9)

    • Yezreeli (4), Lo-ruhama (6), na Lo-ami (9)

  • Tumaini la kurudishwa na kuwa na umoja (10, 11)

1  Neno la Yehova lililomjia Hosea* mwana wa Beeri katika siku za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mfalme wa Israeli.  Yehova alipoanza kusema neno lake kupitia Hosea, Yehova alimwambia hivi Hosea: “Nenda, muoe mwanamke kahaba* na uzae watoto wa ukahaba,* kwa sababu nchi imeacha kabisa kumfuata Yehova kwa sababu ya ukahaba.”*+  Basi akaenda na kumwoa Gomeri binti ya Diblaimu, na Gomeri akapata mimba na kumzalia mwana.  Kisha Yehova akamwambia Hosea: “Mpe mwana huyo jina Yezreeli,* kwa sababu baada ya muda mfupi tu nitaifanya nyumba ya Yehu+ iwajibike kwa sababu ya matendo ya umwagaji wa damu ya Yezreeli, nami nitaukomesha utawala wa wafalme wa Israeli.+  Siku hiyo nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la* Yezreeli.”  Gomeri akapata mimba tena na kuzaa binti. Mungu akamwambia Hosea: “Mpe binti huyo jina Lo-ruhama,* kwa maana sitaionyesha tena rehema+ nyumba ya Israeli, kwa sababu kwa hakika nitawafukuza.+  Lakini nitaionyesha rehema nyumba ya Yuda,+ nami nitawaokoa kwa nguvu za Yehova Mungu wao;+ sitawaokoa kwa upinde au kwa upanga au kwa vita au kwa farasi au kwa wapanda farasi.”+  Baada ya kumwachisha Lo-ruhama kunyonya, Gomeri alipata mimba na kuzaa mwana.  Kisha Mungu akasema: “Mpe mwana huyo jina Lo-ami,* kwa sababu ninyi si watu wangu nami sitakuwa Mungu wenu. 10  “Na Waisraeli* watakuwa wengi kama chembe za mchanga wa bahari, ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na mahali ambapo Mungu aliwaambia, ‘Ninyi si watu wangu,’+ atawaita, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+ 11  Na watu wa Yuda na wa Israeli watakusanywa pamoja ili wawe na umoja+ nao watajichagulia kiongozi mmoja na kupanda kutoka nchini, kwa maana siku ya Yezreeli itakuwa kuu.+

Maelezo ya Chini

Ufupisho wa jina Hoshaya, linalomaanisha “Aliyeokolewa na Yah; Yah Ameokoa.”
Au “malaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Maana yake “Mungu Atapanda Mbegu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Maana yake “Hajaonyeshwa Rehema.”
Maana yake “Si Watu Wangu.”
Yaani, wana wa Israeli.