Hosea 10:1-15

  • Waisraeli ni mzabibu ulioharibika, wataangamizwa (1-15)

10  “Waisraeli ni mzabibu ulioharibika* unaozaa matunda.+ Kadiri matunda yao yanavyoongezeka, ndivyo wanavyozidisha madhabahu zao;+Kadiri nchi yao inavyozaa vizuri, ndivyo fahari ya nguzo zao takatifu inavyozidi kuongezeka.+   Moyo wao una unafiki;*Sasa watapatikana na hatia. Kuna yule atakayebomoa madhabahu zao na kuharibu nguzo zao.   Watasema, ‘Hatuna mfalme,+ kwa sababu hatujamwogopa Yehova. Na mfalme atatufanyia nini?’   Wanasema maneno matupu, wanatoa viapo vya uwongo,+ na kufanya maagano;Basi maamuzi wanayofanya ni kama magugu yenye sumu kwenye mitaro iliyo shambani.+   Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya ndama ya Beth-aveni.+ Watu wake wataiombolezea,Na pia makuhani wa mungu huyo wa kigeni waliokuwa wakiishangilia pamoja na utukufu wake,Kwa maana itachukuliwa na kupelekwa uhamishoni.   Itapelekwa Ashuru kama zawadi kwa mfalme mkuu.+ Waefraimu wataaibishwa,Na Waisraeli wataaibika kwa sababu ya ushauri waliofuata.+   Watu wa Samaria na mfalme wao hakika wataangamizwa,*+Kama kijiti kilichokwanyuliwa kinachoelea juu ya maji.   Mahali pa juu pa Beth-aveni,+ dhambi ya Waisraeli,+ pataharibiwa kabisa.+ Miiba na michongoma itamea juu ya madhabahu zao.+ Watu wataiambia milima, ‘Tufunikeni!’ Na vilima, ‘Tuangukieni!’+   Enyi Waisraeli, mmetenda dhambi tangu kule Gibea.+ Nao wanaendelea kutenda dhambi huko. Vita havikuwaangamiza kabisa wana wa ukosefu wa uadilifu kule Gibea. 10  Pia nitawatia nidhamu wakati ninaopenda. Na mataifa yatakusanyika dhidi yao,Makosa yao mawili yatakapofungiliwa juu yao.* 11  Waefraimu walikuwa kama ndama jike aliyezoezwa aliyependa kupura,Basi niliihurumia shingo yake nzuri. Sasa nitamfanya mtu fulani apande juu ya Waefraimu na kuwaendesha.*+ Watu wa Yuda watalima; watu wa Yakobo watamlimia. 12  Jipandieni mbegu kwa uadilifu na mvune upendo mshikamanifu. Jilimieni shamba linalofaa kwa kilimo+Maadamu wakati upo wa kumtafuta Yehova,+Mpaka atakapokuja na kuwafundisha uadilifu.+ 13  Lakini mmelima uovu,Mmevuna ukosefu wa uadilifu,+Nanyi mmekula matunda ya udanganyifu;Kwa sababu mmetumaini njia yenu wenyewe,Mmewatumaini mashujaa wenu wengi. 14  Fujo itatokea dhidi ya watu wenu,Na majiji yenu yenye ngome yataharibiwa yote,+Kama Shalmani alivyoharibu kabisa nyumba ya Arbeli,Katika siku ya vita, akina mama walipondwapondwa pamoja na watoto wao. 15  Hivyo ndivyo mtakavyotendewa, enyi wakaaji wa Betheli,+ kwa sababu ya uovu wenu uliozidi. Kwa hakika mfalme wa Israeli ataangamizwa* wakati wa mapambazuko.”+

Maelezo ya Chini

Au labda, “unaoenea.”
Au “hila; udanganyifu.”
Tnn., “watanyamazishwa.”
Yaani, watakapobeba adhabu yao kama nira.
Au “kuwafunga nira.”
Tnn., “atanyamazishwa.”