Hosea 12:1-14

  • Waefraimu wanapaswa kumrudia Yehova (1-14)

    • Yakobo alishindana na Mungu (3)

    • Yakobo alimlilia Mungu ili ambariki (4)

12  “Waefraimu wanakula upepo. Wanaukimbiza upepo wa mashariki siku nzima. Wanazidisha uwongo na ukatili. Wanafanya agano na Ashuru+ na kupeleka mafuta Misri.+   Yehova ana kesi dhidi ya watu wa Yuda;+Atawafanya wazao wa Yakobo wawajibike kulingana na njia zao,Naye atawalipa kulingana na matendo yao.+   Wakiwa tumboni, Yakobo alimshika kisigino ndugu yake,+Na kwa nguvu zake alishindana na Mungu.+   Aliendelea kushindana na malaika na kumshinda. Alilia na kumsihi apate kibali chake.”+ Alimkuta Yakobo kule Betheli, na huko akazungumza nasi,+   Yehova Mungu wa majeshi,+Yehova ndilo jina lake la ukumbusho.*+   “Basi mrudieni Mungu wenu,+Dumisheni upendo mshikamanifu na haki,+Na sikuzote mumtumaini Mungu wenu.   Lakini mfanyabiashara ana mizani ya udanganyifu mkononi mwake;Anapenda kuwapunja watu.+   Waefraimu husema, ‘Kwa kweli, tumetajirika;+Tumepata utajiri.+ Na katika kazi zetu zote za jasho, hawatapata kosa au dhambi yoyote.’   Lakini mimi ni Yehova Mungu wenu kuanzia* mlipokuwa nchini Misri.+ Nitawafanya mkae tena katika mahemaKama ilivyokuwa katika siku za kipindi kilichoamriwa.* 10  Niliongea na manabii,+Nikazidisha maono yao,Nami nikasimulia mifano kupitia manabii. 11  Kule Gileadi watu wametenda kwa udanganyifu*+ na uwongo. Huko Gilgali wametoa dhabihu za ng’ombe dume,+Na madhabahu zao ni kama marundo ya mawe katika mitaro iliyo shambani.+ 12  Yakobo alikimbilia eneo* la Aramu;*+Israeli+ alitumikia huko ili apate mke,+Na ili apate mke, alichunga kondoo.+ 13  Na kupitia nabii, Yehova aliwapandisha Waisraeli kutoka Misri,+Na kupitia nabii, walilindwa.+ 14  Waefraimu wamemchukiza sana Mungu;+Wataendelea kuwa na hatia ya damu;Bwana wao atawaadhibu kwa sababu ya kumwaibisha.”+

Maelezo ya Chini

Au “anakumbukwa kwa jina hilo.”
Au labda, “sherehe.”
Au “tangu.”
Au “wametenda uchawi; mazingaombwe.”
Tnn., “shamba.”
Au “Siria.”