Hosea 13:1-16

  • Waefraimu waabudu sanamu na kumsahau Yehova (1-16)

    • “Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?” (14)

13  “Waefraimu walipoongea, watu walitetemeka;Walikuwa maarufu miongoni mwa Waisraeli.+ Lakini wakawa na hatia kuhusiana na Baali,+ nao wakafa.   Sasa wanazidisha dhambi yaoNa kutengeneza sanamu za madini* kwa fedha yao;+Wanatengeneza sanamu kwa ustadi, hizo zote ni kazi za mafundi. Wanasema hivi mbele ya sanamu hizo: ‘Watu wanaotoa dhabihu na wabusu ndama hawa.’+   Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,Kama umande unaotoweka mapema,Kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba kutoka kwenye uwanja wa kupuria,Na kama moshi unaotoka katika bomba la moshi paani.   Lakini mimi ni Yehova Mungu wenu kuanzia* mlipokuwa nchini Misri;+Hamkumjua Mungu mwingine yeyote isipokuwa mimi,Na hakuna mwokozi mwingine yeyote ila mimi.+   Niliwajua mlipokuwa nyikani,+ katika nchi yenye ukame.   Walitosheka na malisho yao,+Walitosheka moyo wao ukawa na kiburi. Na kwa hiyo wakanisahau.+   Nitakuwa kama mwanasimba kwao,+Kama chui anayevizia njiani.   Nitawarukia kama dubu aliyepoteza watoto wake,Nami nitavirarua vifua vyao.* Na huko nitawanyafua kama simba;Mnyama wa mwituni atawararua vipandevipande.   Atawaangamiza, enyi Waisraeli,Kwa sababu mmenigeuka, mmemgeuka msaidizi wenu. 10  Yuko wapi sasa mfalme wenu ili awaokoe katika majiji yenu yote,+Na watawala* wenu ambao mlisema kuwahusu,‘Tupe mfalme na wakuu’?+ 11  Kwa hasira nikawapa mfalme,+Nami nitamwondoa kwa ghadhabu.+ 12  Kosa la Waefraimu limefungwa kabisa;*Dhambi yao imewekwa akiba. 13  Watashikwa na uchungu wa kuzaa. Lakini wao ni mtoto asiye na hekima;Hatoki tumboni wakati wa kuzaliwa ufikapo. 14  Nitawakomboa kutoka katika nguvu za Kaburi;*Nitawaokoa kutoka katika kifo.+ Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?*+ Ewe Kaburi, yako wapi maangamizi yako?+ Macho yangu yatazuiwa yasione huruma. 15  Hata wakisitawi kati ya matete,Upepo wa mashariki utakuja, upepo wa Yehova,Utakuja kutoka jangwani, kukausha kisima chao na chemchemi yao. Huyo atapora hazina ya vitu vyao vyote vyenye thamani.+ 16  Watu wa Samaria watahesabiwa kuwa na hatia,+ kwa sababu wamemwasi Mungu wao.+ Watauawa kwa upanga,+Watoto wao watapondwapondwa,Na wanawake wao wenye mimba watapasuliwa tumbo.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “za kuyeyushwa.”
Au “tangu.”
Tnn., “chumba cha moyo wao.”
Tnn., “waamuzi.”
Au “limehifadhiwa.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “iko wapi michomo yako?”