Hosea 14:1-9

  • Wasihiwa wamrudie Yehova (1-3)

    • Kutoa sifa ya midomo (2)

  • Waisraeli waponywa, hawatakosa uaminifu tena (4-9)

14  “Enyi Waisraeli, mrudieni Yehova Mungu wenu,+Kwa maana mmejikwaa kwa sababu ya kosa lenu.   Mrudieni Yehova kwa maneno haya,Mwambieni, ‘Tusamehe kosa letu+ na ukubali yaliyo mema,Nasi tutatoa sifa ya midomo yetu+ kama vile ambavyo tungetoa ng’ombe dume wachanga.*   Ashuru haitatuokoa.+ Hatutapanda farasi,+Na hatutaziambia tena kazi za mikono yetu, “Ee Mungu wetu!” Kwa sababu ni wewe unayemwonyesha yatima rehema.’+   Nitauponya ukosefu wao wa uaminifu.+ Nitawapenda kwa hiari yangu mwenyewe,+Kwa sababu hasira yangu imegeuka na kuwaacha.+   Nitakuwa kama umande kwa Waisraeli;Watachanua kama yungiyungiNao wataipenyeza chini mizizi yao kama miti ya Lebanoni.   Vitawi vyao vitasambaa,Fahari yao itakuwa kama ya mzeituni,Na manukato yao kama ya Lebanoni.   Watakaa tena chini ya kivuli chake. Watapanda nafaka na kutokeza matumba kama mzabibu.+ Umaarufu* wao utakuwa kama wa divai ya Lebanoni.   Waefraimu watasema, ‘Tunahitaji tena sanamu za nini?’+ Nitawajibu na kuwalinda.+ Nitakuwa kama mberoshi unaositawi. Mtapata matunda yenu kutoka kwangu.”   Ni nani aliye na hekima? Na aelewe mambo haya. Ni nani aliye na busara? Na ayajue mambo hayo. Kwa maana njia za Yehova zimenyooka,+Na waadilifu watatembea katika njia hizo;Lakini watenda dhambi watajikwaa humo.

Maelezo ya Chini

Tnn., “nasi tutakutolea ng’ombe dume wachanga wa midomo yetu.”
Tnn., “Ukumbusho.”