Hosea 4:1-19

  • Kesi ya Yehova dhidi ya Waisraeli (1-8)

    • Watu hawamjui Mungu nchini (1)

  • Waisraeli waabudu sanamu na kufanya ukahaba (9-19)

    • Wapotoshwa na roho ya ukahaba (12)

4  Lisikieni neno la Yehova, enyi Waisraeli,Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya wakaaji wa nchi,+Kwa sababu hakuna ukweli wala upendo mshikamanifu wala ujuzi kumhusu Mungu nchini.+   Viapo vya uwongo na udanganyifu+ na mauaji+Na wizi na uzinzi+ umeenea sana,Na tendo moja la umwagaji wa damu linafuata tendo lingine la umwagaji wa damu.+   Ndiyo sababu nchi itaomboleza+Na kila mkaaji nchini atadhoofika;Wanyama wa mwituni na ndege wa angani,Hata samaki wa baharini, wataangamia.   “Hata hivyo, mtu yeyote asibishane nanyi wala kuwakaripia,+Kwa maana watu wenu ni kama wale wanaobishana na kuhani.+   Basi mtajikwaa kweupe kabisa wakati wa mchana,Na nabii atajikwaa pamoja nanyi, kana kwamba ni usiku. Nami nitamnyamazisha* mama yenu.   Watu wangu watanyamazishwa,* kwa sababu hawana ujuzi. Kwa sababu mmekataa ujuzi,+Nitawakataa pia msinitumikie mkiwa makuhani wangu;Na kwa sababu mmesahau sheria* ya Mungu wenu,+Mimi mwenyewe nitawasahau wana wenu.   Kadiri walivyoongezeka,* ndivyo walivyozidi kunitendea dhambi.+ Nitabadili utukufu wao uwe aibu.*   Wanajilisha dhambi ya watu wangu,Nao wana pupa ya kuona watu wangu wakikosea.   Yatakayowapata watu ndiyo yatakayompata kuhani;Nitawafanya wawajibike kwa sababu ya njia zao,Nami nitawaletea matokeo ya matendo yao.+ 10  Watakula lakini hawatashiba.+ Watafanya ngono ovyovyo,* lakini hawataongezeka,+Kwa sababu hawajamheshimu Yehova. 11  Ukahaba* na divai na divai mpyaHuondoa kichocheo cha kutenda lililo jema.*+ 12  Watu wangu hutafuta ushauri kutoka kwa sanamu zao za miti,Wakifanya mambo wanayoambiwa na fimbo yao;*Kwa sababu roho ya ukahaba* huwapotosha,Na kwa ukahaba* wao wanakataa kujinyenyekeza kwa Mungu wao. 13  Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima,+Na juu ya vilima wanafukiza moshi wa dhabihu,Chini ya mialoni na milubna na kila mti mkubwa,+Kwa sababu vivuli vyake ni vizuri. Ndiyo sababu mabinti wenu wanafanya ukahaba*Na mabinti wakwe zenu wanafanya uzinzi. 14  Sitawafanya mabinti wenu wawajibike kwa sababu ya ukahaba* wao,Wala mabinti wakwe zenu kwa sababu ya uzinzi wao. Kwa maana wanaume huwatafuta makahabaNao hutoa dhabihu pamoja na makahaba wa hekaluni;Watu kama hao wasio na uelewaji+ wataangamia. 15  Ingawa mnafanya ukahaba,* enyi Waisraeli,+Watu wa Yuda wasiwe na hatia.+ Msije Gilgali+ wala Beth-aveni,+Na msiape mkisema, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’+ 16  Waisraeli wamekuwa wakaidi kama ng’ombe mkaidi.+ Je, sasa Yehova atawachunga kama mwanakondoo dume malishoni?* 17  Waefraimu wameshikamana na sanamu.+ Waacheni! 18  Pombe yao* inapomalizika,Wanafanya ngono ovyovyo.* Na watawala wao* hupenda sana aibu.+ 19  Upepo utawafunga katika mabawa yake,*Nao watazionea aibu dhabihu zao.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “nitamwangamiza.”
Tnn., “wataangamizwa.”
Au “mafundisho.”
Yaani, makuhani.
Au labda, “Wameniaibisha badala ya kunitukuza.”
Au “Watakuwa waasherati kupindukia; Watafanya umalaya.”
Tnn., “Huondoa moyo.”
Au “Umalaya.”
Au “fimbo yao ya ubashiri.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Tnn., “mahali penye nafasi ya kutosha.”
Au “Pombe yao ya ngano.”
Au “Wanafanya uasherati kupindukia; Wanafanya ukahaba.”
Tnn., “ngao zao.”
Au “utawafagilia mbali.”