Hosea 5:1-15

  • Waefraimu na watu wa Yuda wahukumiwa (1-15)

5  “Sikieni jambo hili, enyi makuhani,+Sikiliza kwa makini, Ee nyumba ya Israeli,Sikiliza, Ee nyumba ya mfalme,Kwa maana hukumu inawahusu ninyi;Kwa sababu ninyi ni mtego kwa MispaNa wavu uliotandazwa juu ya Tabori.+   Na wale wanaoanguka* wamezama ndani kabisa* katika mauaji,Nami ninawaonya* wote.   Ninawajua Waefraimu,Na Waisraeli hawajafichika mbele zangu. Kwa maana sasa, enyi Waefraimu, mmefanya ngono ovyoovyo;*Waisraeli wamejichafua wenyewe.+   Shughuli zao haziwaruhusu wamrudie Mungu wao,Kwa sababu kuna roho ya ukahaba* miongoni mwao;+Nao hawamtambui Yehova.   Kiburi cha Waisraeli kimetoa ushahidi dhidi yao;*+Waisraeli na Waefraimu wamejikwaa katika kosa lao,Na watu wa Yuda wamejikwaa pamoja nao.+   Walienda kumtafuta Yehova wakiwa na kundi lao la kondoo na kundi lao la ng’ombe,Lakini hawakuweza kumpata. Alikuwa amejitenga mbali nao.+   Wamemsaliti Yehova,+Kwa sababu wamekuwa baba za wana wa kigeni. Sasa mwezi mmoja utawanyafua* pamoja na mafungu* yao.   Pigeni pembe+ huko Gibea, tarumbeta huko Rama!+ Pigeni kelele za vita huko Beth-aveni+—tunawafuata, enyi Wabenjamini!   Enyi Waefraimu, mtakuwa kitu cha kutisha katika siku ya adhabu.+ Nimetangaza jambo ambalo hakika litatukia miongoni mwa makabila ya Israeli. 10  Wakuu wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mpaka.+ Nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji. 11  Waefraimu wamekandamizwa, wamepondwa na hukumu,Kwa maana waliazimia kumfuata adui yao.+ 12  Kwa hiyo nilikuwa kama nondo* kwa WaefraimuNa kama uozo kwa nyumba ya Yuda. 13  Waefraimu walipoona ugonjwa wao, na watu wa Yuda kidonda chao,Waefraimu walienda Ashuru+ na kutuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya,Wala hakuweza kuponya kidonda chenu. 14  Kwa maana nitakuwa kama mwanasimba kwa Waefraimu,Na kama simba mwenye nguvu* kwa nyumba ya Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua vipandevipande na kwenda zangu;+Nitawabeba na kwenda nao, na hakuna yeyote atakayewaokoa.+ 15  Nitaenda na kurudi mahali pangu mpaka watakapolipia hatia yao,Na kisha watatafuta kibali changu.*+ Watakapokuwa wakiteseka, watanitafuta.”+

Maelezo ya Chini

Au “waasi.”
Au “wamejitumbukiza kabisa.”
Au “nitawatia nidhamu.”
Au “mmefanya uasherati; mmefanya umalaya.”
Au “umalaya.”
Tnn., “mbele za uso wao.”
Au labda, “Watanyafuliwa katika mwezi mmoja.”
Au “mashamba yao.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Tnn., “uso wangu.”