Hosea 6:1-11
6 “Njooni, tumrudie Yehova,Kwa maana ameturarua vipandevipande,+ lakini atatuponya.
Alitupiga, lakini atafunga majeraha yetu.
2 Atatuhuisha baada ya siku mbili.
Siku ya tatu atatuinua,Nasi tutaishi mbele zake.
3 Tutamjua, tutajitahidi kumjua Yehova.
Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko;Atakuja kwetu kama mvua kubwa,Kama mvua ya masika inayolowesha dunia.”
4 “Niwafanyie nini, enyi Waefraimu?
Niwafanyie nini, enyi watu wa Yuda,Kwa maana upendo wenu mshikamanifu ni kama ukungu wa asubuhi,Kama umande unaotoweka haraka.
5 Ndiyo sababu nitawakatakata kabisa kwa kutumia manabii;+Nitawaua kwa maneno ya kinywa changu.+
Na hukumu zangu dhidi yenu zitang’aa kama mwangaza.+
6 Kwa maana ninapendezwa na upendo mshikamanifu,* si dhabihu,Na kumjua Mungu, badala ya dhabihu nzima za kuteketezwa.+
7 Lakini wao, kama wanadamu tu, wamevunja agano.+
Wamenisaliti katika nchi yao.
8 Gileadi ni mji wa watenda maovu,+Umefunikwa kwa nyayo za damu.+
9 Magenge ya makuhani ni kama makundi ya wavamizi yanayomvizia mtu.
Wanawaua watu barabarani kule Shekemu,+Kwa maana mwenendo wao ni wa aibu.
10 Nimeona jambo la kuchukiza sana katika nyumba ya Israeli.
Huko Waefraimu hufanya ukahaba;+Waisraeli wamejichafua wenyewe.+
11 Zaidi ya hayo, enyi watu wa Yuda, wakati wa mavuno umetengwa kwa ajili yenu,Nitakapowakusanya watu wangu waliotekwa.”+
Maelezo ya Chini
^ Au “rehema.”