Hosea 8:1-14

  • Matokeo ya kuabudu sanamu (1-14)

    • Kupanda upepo, kuvuna kimbunga (7)

    • Waisraeli wamemsahau Muumba wao (14)

8  “Pigeni pembe!+ Adui anakuja kama tai kuivamia nyumba ya Yehova,+Kwa sababu wamelivunja agano langu+ na kuasi sheria yangu.+   Wananililia wakisema, ‘Mungu wetu, sisi, Waisraeli, tunakujua!’+   Waisraeli wamekataa mema.+ Adui na awafuatie.   Wamejichagulia wafalme, lakini bila kibali changu. Wamejichagulia wakuu, lakini sikuwatambua. Wametengeneza sanamu kwa fedha yao na dhahabu yao,+Wakajiletea maangamizi.+   Ndama wenu amekataliwa, enyi watu wa Samaria.+ Hasira yangu inawaka dhidi yao.+ Wataendelea mpaka lini kushindwa kuwa bila hatia?*   Kwa maana ndama huyu ametoka Israeli. Fundi ndiye aliyemtengeneza, si Mungu;Ndama wa Samaria atavunjwa na kubaki vipandevipande.   Kwa maana wanapanda upepo,Nao watavuna kimbunga.+ Hakuna bua linalozaa nafaka iliyokomaa;+Bua lolote linalochipuka halitokezi unga. Unga wowote wanaopata, utamezwa na wageni.+   Waisraeli watamezwa.+ Sasa watakuwa miongoni mwa mataifa,+Kama chombo ambacho hakitakikani.   Kwa maana wamepanda kwenda Ashuru,+ kama punda mwitu aliye peke yake. Waefraimu wamekodi wapenzi.+ 10  Ingawa wanawakodi kutoka miongoni mwa mataifa,Sasa mimi nitawazingira;Wataanza kuteseka+ kwa sababu ya mzigo waliotwikwa na mfalme na wakuu. 11  Kwa maana Waefraimu wamezidisha madhabahu ili watende dhambi.+ Zikawa madhabahu walizotumia kutenda dhambi.+ 12  Niliwaandikia mambo mengi ya sheria* yangu,Lakini waliyaona kuwa mambo ya ajabu.+ 13  Wananitolea zawadi za dhabihu, nao wanakula nyama,Lakini mimi Yehova sipendezwi nazo.+ Sasa nitakumbuka kosa lao na kuwaadhibu kwa sababu ya dhambi zao.+ Wamegeuka na kurudi* Misri.+ 14  Waisraeli wamemsahau Muumba wao+ na kujenga mahekalu,+Na watu wa Yuda wamezidisha majiji yenye ngome.+ Lakini nitashusha moto kwenye majiji yao,Nao utateketeza minara iliyo katika kila jiji.”+

Maelezo ya Chini

Au “kushindwa kuwa safi?”
Au “mafundisho.”
Au labda, “Watarudi.”