Hosea 9:1-17

  • Mungu awakataa Waefraimu kwa sababu ya dhambi zao (1-17)

    • Wajiweka wakfu kwa mungu anayechukiza (10)

9  “Msishangilie, enyi Waisraeli,+Msishangilie kama mataifa. Kwa maana kwa ukahaba* wenu mmetangatanga na kumwacha Mungu wenu.+ Mmependa malipo ya kahaba katika kila kiwanja cha kupuria nafaka.+   Lakini uwanja wa kupuria na shinikizo la divai havitawalisha,Na divai mpya itawaishia.+   Hawataendelea kukaa katika nchi ya Yehova;+Badala yake, Waefraimu watarudi Misri,Nao watakula vitu visivyo safi kule Ashuru.+   Hawatammiminia tena Yehova matoleo ya divai;+Dhabihu zao hazitampendeza.+ Dhabihu hizo ni kama mkate wa maombolezo;Wote wanaoula watajichafua. Kwa maana mkate wao ni wao peke yao;*Hautaletwa katika nyumba ya Yehova.   Mtafanya nini katika siku ya mkutano,*Katika siku ya sherehe ya Yehova?   Kwa maana tazama! watalazimika kukimbia kwa sababu ya maangamizi.+ Misri itawakusanya pamoja,+ na Memfisi itawazika.+ Upupu utamiliki vitu vyao vya fedha vyenye thamani,Na vichaka vya miiba vitakuwa katika mahema yao.   Siku za kuwajibika zitakuja,+Siku za kulipiza kisasi zitakuja,Na Waisraeli watajua jambo hilo. Nabii wao atakuwa mjinga, na mtu anayeongozwa na roho atashikwa na wazimu;Kwa sababu makosa yenu ni mengi, uhasama dhidi yenu ni mkubwa.”   Mlinzi+ wa Efraimu alikuwa na Mungu wangu.+ Lakini sasa njia zote za manabii wake+ ni kama mitego ya mwindaji wa ndege;Kuna uhasama katika nyumba ya Mungu wake.   Wamezama ndani sana katika maangamizi, kama ilivyokuwa kule Gibea.+ Atakumbuka kosa lao na kuwaadhibu kwa sababu ya dhambi zao.+ 10  “Niliwapata Waisraeli kama zabibu nyikani.+ Kama matunda ya kwanza ya tini niliwaona mababu zenu. Lakini walienda kwa Baali wa Peori;+Walijiweka wakfu kwa kile kitu cha aibu,*+Wakawa chukizo kama kitu walichokipenda. 11  Utukufu wa Waefraimu unaruka mbali kama ndege;Hakuna kuzaa, hakuna mimba, na hakuna kushika mimba.+ 12  Hata wakiwalea watoto,Nitawaangamiza asibaki mtu yeyote;+Naam, ole wao nitakapowaacha!+ 13  Waefraimu, waliopandwa malishoni, walikuwa kama Tiro kwangu;+Sasa lazima Waefraimu wawalete wana wao ili wachinjwe.” 14  Ee Yehova, wape unachopaswa kuwapa;Tumbo la uzazi linaloharibu mimba na matiti yaliyokauka.* 15  “Walifanya uovu wao wote kule Gilgali,+ kwa maana nilianza kuwachukia huko. Nitawafukuza katika nyumba yangu kwa sababu ya matendo yao maovu.+ Sitawapenda tena;+Wakuu wao wote ni wakaidi. 16  Waefraimu wataangushwa chini.+ Mzizi wao utakauka, nao hawatazaa tunda lolote. Hata wakizaa, nitawaua wazao wao wanaowapenda.” 17  Mungu wangu atawakataa,Kwa maana hawajamsikiliza,+Nao watakuwa wakimbizi miongoni mwa mataifa.+

Maelezo ya Chini

Au “umalaya.”
Au “ni wa nafsi yao wenyewe.”
Au “karamu yenu iliyoamriwa.”
Au “mungu wa aibu.”
Au “yaliyonyauka.”