Maombolezo 1:1-22

  • Jiji la Yerusalemu lafananishwa na mjane

    • Limebaki ukiwa na kuachwa (1)

    • Dhambi nzito sana za Sayuni (8, 9)

    • Sayuni lakataliwa na Mungu (12-15)

    • Hakuna wa kulifariji Sayuni (17)

א [Aleph]* 1  Lo! Jiji lililokuwa limejaa watu+ sasa limebaki ukiwa! Limekuwa kama mjane, jiji lililokuwa na watu wengi miongoni mwa mataifa!+ Jiji lililokuwa binti ya mfalme kati ya mikoa* limefanywa kuwa mtumwa!+ ב [Beth]   Binti huyo analia sana usiku,+ na machozi yake yamefunika mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji.+ Marafiki zake wote wamemsaliti;+ wamekuwa maadui wake. ג [Gimel]   Yuda amepelekwa uhamishoni+ kwa mateso na utumwa wa kikatili.+ Ni lazima akae miongoni mwa mataifa;+ hana mahali pa kupumzika. Wote waliokuwa wakimtesa wamemkabili katika mateso yake. ד [Daleth]   Barabara zinazoelekea Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna yeyote anayekuja kwenye sherehe.+ Malango yake yote yamebaki ukiwa;+ makuhani wake wanalia kwa uchungu. Mabikira* wake wanaomboleza, naye analia kwa maumivu makali. ה [He]   Wapinzani wake sasa ni mabwana wakubwa wake; maadui wake hawajali.+ Kwa maana Yehova amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi.+ Adui amewapeleka watoto wake utekwani.+ ו [Waw]   Fahari yote ya binti ya Sayuni imetoweka.+ Wakuu wake ni kama paa dume waliokosa malisho,Nao wanatembea kwa uchovu mbele ya yule anayewafuatia. ז [Zayin]   Katika siku za mateso yake na za kukosa makao, Yerusalemu hukumbukaVitu vyote vyenye thamani vilivyokuwa vyake siku za zamani za kale.+ Watu wake walipotiwa mikononi mwa adui, naye hakuwa na msaidizi,+Maadui walimwona na kumcheka* alipoanguka.+ ח [Heth]   Yerusalemu ametenda dhambi nzito sana.+ Ndiyo sababu amekuwa kitu kinachochukiza sana. Wote waliokuwa wakimheshimu sasa wanamtendea kama kitu kinachodharauliwa, kwa maana wameuona uchi wake.+ Yeye mwenyewe analia kwa maumivu+ na kujificha kwa aibu. ט [Teth]   Uchafu wake umo ndani ya mavazi yake. Hakufikiria wakati wake ujao.+ Alianguka kwa njia ya kushangaza; hana yeyote wa kumfariji. Ee Yehova, yaangalie mateso yangu, kwa sababu adui amejitukuza.+ י [Yod] 10  Adui amechukua hazina zake zote.+ Kwa maana ameona* mataifa yakiingia mahali pake patakatifu,+Watu ulioamuru wasiingie katika kutaniko lako. כ [Kaph] 11  Watu wake wote wanalia kwa uchungu; wanatafuta mkate.+ Wamewapa vitu vyao vyenye thamani ili wapate kitu cha kula, angalau waendelee kuishi.* Tazama, Ee Yehova, uone kwamba nimekuwa kama mwanamke asiyefaa kitu.* ל [Lamed] 12  Enyi nyote mnaopita njiani, mateso yangu kwenu si kitu? Tazameni mwone! Je, kuna maumivu kama maumivu niliyoletewa,Ambayo Yehova aliniletea katika siku ya hasira yake kali?+ מ [Mem] 13  Kutoka juu sana ameushusha moto mifupani mwangu,+ naye anautiisha kila mfupa. Ametandaza wavu wa kunasa miguu yangu; amenilazimisha nirudi nyuma. Amenifanya kuwa mwanamke aliye ukiwa. Mchana kutwa mimi ni mgonjwa. נ [Nun] 14  Dhambi zangu zimefungwa kama nira, mkono wake umezifunga pamoja. Zimewekwa shingoni mwangu, nami nimeishiwa na nguvu. Yehova amenitia mikononi mwa watu ambao siwezi kuwapinga.+ ס [Samekh] 15  Yehova amewatupa pembeni watu wote wenye nguvu kati yangu.+ Ameukusanya umati wa watu dhidi yangu ili kuwaponda vijana wangu wa kiume.+ Yehova amemkanyaga binti bikira wa Yuda katika shinikizo la divai.+ ע [Ayin] 16  Ninalia kwa sababu ya mambo haya;+ macho yangu yanatiririka machozi. Kwa maana yeyote ambaye angenifariji au kuniburudisha yuko mbali sana nami. Wanangu wamebaki ukiwa, kwa maana adui ameshinda. פ [Pe] 17  Sayuni amenyoosha mikono yake;+ hana wa kumfariji. Yehova amewaagiza maadui wote wanaomzunguka Yakobo wamshambulie.+ Yerusalemu limekuwa kitu cha kuchukiza sana kwao.+ צ [Tsade] 18  Yehova ni mwadilifu,+ kwa kuwa nimeasi amri zake.*+ Sikilizeni, enyi mataifa yote, mwone maumivu yangu. Mabikira* wangu na vijana wangu wa kiume wamepelekwa utekwani.+ ק [Qoph] 19  Nimewaita wapenzi wangu, lakini wamenisaliti.+ Makuhani wangu na wazee wangu wameangamia jijini,Walipokuwa wakitafuta chakula ili waendelee kuishi.*+ ר [Resh] 20  Tazama, Ee Yehova, kwa maana ninateseka sana. Matumbo yangu yanasukasuka. Moyo wangu umepinduka ndani yangu, kwa maana nimekuwa mwasi kabisa.+ Nje, upanga unaangamiza;+ ndani ya nyumba, ni kama kifo. ש [Shin] 21  Watu wamesikia kilio changu cha uchungu; hakuna yeyote wa kunifariji. Maadui wangu wote wamesikia kuhusu msiba wangu.+ Wanashangilia, kwa sababu uliuleta. Lakini utaleta siku uliyotangaza,+ wakati huo watakuwa kama mimi.+ ת [Taw] 22  Uovu wao wote na uje mbele zako, na uwatese vikali,+Kama tu ulivyonitesa vikali kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kwa maana vilio vyangu vya uchungu ni vingi, na moyo wangu ni mgonjwa.

Maelezo ya Chini

Sura ya 1-4 ni nyimbo za maombolezo zilizoandikwa kwa kufuata alfabeti ya Kiebrania au mpangilio wa kishairi.
Au “wilaya za utawala.”
Au “Wanawali.”
Au “kumdhihaki.”
Yaani, watu wa Yerusalemu.
Au “wahuishe nafsi.”
Jiji la Yerusalemu linafananishwa na mwanamke.
Tnn., “nimekiasi kinywa chake.”
Au “Wanawali.”
Au “waihuishe nafsi.”