Maombolezo 4:1-22

  • Matokeo mabaya ya kuzingirwa kwa Yerusalemu

    • Ukosefu wa chakula (4, 5, 9)

    • Wanawake wawachemsha watoto wao wenyewe (10)

    • Yehova amemwaga hasira yake (11)

א [Aleph] 4  Jinsi dhahabu inayong’aa ilivyopoteza mng’ao wake, dhahabu bora!+ Jinsi mawe matakatifu+ yalivyotapakaa kwenye kila pembe ya barabara!+ ב [Beth]   Na wana wa Sayuni wenye thamani, ambao walipimwa kwa uzito wa* dhahabu safi,Sasa wanaonwa kuwa kama magudulia ya udongo,Kazi ya mikono ya mfinyanzi! ג [Gimel]   Hata mbwamwitu huwapa watoto wao matiti wanyonye,Lakini binti ya watu wangu amekuwa mkatili,+ kama mbuni nyikani.+ ד [Daleth]   Ulimi wa mtoto anayenyonya hushikamana na kaakaa lake kwa sababu ya kiu. Watoto wadogo wanaombaomba mikate,+ lakini hakuna anayewapa.+ ה [He]   Wale waliokuwa wakila vyakula vitamu wanalala barabarani kwa sababu ya njaa kali.+ Wale waliolelewa wakivaa mavazi mekundu+ wamekumbatia marundo ya majivu. ו [Waw]   Adhabu* ya binti ya watu wangu ni kubwa kuliko adhabu iliyotolewa kwa sababu ya dhambi ya Sodoma,+Lililopinduliwa haraka, na hakukuwa na mtu wa kulisaidia.*+ ז [Zayin]   Wanadhiri wake+ walikuwa safi kuliko theluji, weupe kuliko maziwa. Walikuwa wekundu kuliko marijani; walikuwa kama vito vya yakuti vilivyong’arishwa. ח [Heth]   Wamekuwa weusi kuliko masizi;*Hawatambuliwi barabarani. Ngozi yao imenyauka juu ya mifupa yao;+ imekuwa kama ukuni uliokauka. ט [Teth]   Waliouawa kwa upanga ni afadhali kuliko waliokufa kwa njaa kali,+Wale wanaokonda, wanaochomwa kana kwamba kwa upanga kwa sababu ya kukosa chakula kutoka shambani. י [Yod] 10  Mikono ya wanawake wenye huruma imewachemsha watoto wao wenyewe.+ Wamekuwa chakula chao cha maombolezo wakati wa kuangamia kwa binti ya watu wangu.+ כ [Kaph] 11  Yehova ameonyesha ghadhabu yake;Amemwaga hasira yake kali.+ Anawasha moto Sayuni unaoteketeza misingi yake.+ ל [Lamed] 12  Wafalme wa dunia na wakaaji wote wa ardhi inayozaa hawakuaminiKwamba mpinzani na adui wangeingia katika malango ya Yerusalemu.+ מ [Mem] 13  Hilo lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, makosa ya makuhani wake,+Waliomwaga damu ya waadilifu waliokuwa katika jiji hilo.+ נ [Nun] 14  Wametangatanga kama vipofu+ barabarani. Wamechafuliwa na damu,+ Hivi kwamba hakuna yeyote anayeweza kuyagusa mavazi yao. ס [Samekh] 15  “Nendeni zenu! Wachafu!” watu wanawaambia kwa sauti. “Nendeni zenu! Nendeni zenu! Msituguse!” Kwa maana hawana makao, nao wanatangatanga. Miongoni mwa mataifa watu wamesema: “Hawawezi kukaa hapa pamoja nasi.*+ פ [Pe] 16  Uso wa Yehova umewatawanya;+Hatawaonyesha tena kibali chake. Watu hawatawaheshimu makuhani,+ hawatawatendea wazee kwa fadhili.”+ ע [Ayin] 17  Hata sasa macho yetu yamechoka kabisa tukitarajia kupata msaada bila mafanikio.+ Tulitarajia na kutarajia kupata msaada kutoka kwa taifa ambalo halingeweza kutuokoa.+ צ [Tsade] 18  Wametuwinda katika kila hatua+ hivi kwamba hatungeweza kutembea kwenye viwanja vya jiji letu. Mwisho wetu umekaribia; siku zetu zimekwisha, kwa maana mwisho wetu umefika. ק [Qoph] 19  Waliotufuatia walikwenda kasi kuliko tai wa angani.+ Walitukimbiza milimani; walituvamia nyikani. ר [Resh] 20  Pumzi ya mianzi ya pua zetu, mtiwa-mafuta wa Yehova,+ amenaswa katika shimo lao kubwa,+Yule tuliyesema hivi kumhusu: “Tutaishi chini ya kivuli chake miongoni mwa mataifa.” ש [Sin] 21  Furahi na kushangilia, Ee binti ya Edomu,+ unayekaa katika nchi ya Usi. Lakini wewe pia utapitishiwa kikombe,+ nawe utalewa na kufunua uchi wako.+ ת [Taw] 22  Adhabu ya dhambi yako, Ee binti ya Sayuni, imekwisha. Hatakupeleka tena uhamishoni.+ Lakini ataukazia uangalifu uovu wako, Ee binti ya Edomu. Atafunua dhambi zako.+

Maelezo ya Chini

Au “waliokuwa na thamani kama.”
Tnn., “bila mkono wa kulisaidia.”
Tnn., “Dhambi.”
Tnn., “weusi.”
Au “kuishi hapa wakiwa wageni.”