Maombolezo 5:1-22

  • Watu wasali warudishwe

    • ‘Kumbuka yale ambayo yametupata’ (1)

    • ‘Ole wetu; tumetenda dhambi’ (16)

    • ‘Turudishe, Ee Yehova’ (21)

    • “Zifanye siku zetu ziwe mpya” (21)

5  Kumbuka, Ee Yehova, yale ambayo yametupata. Tazama na uone aibu yetu.+   Wageni wamepewa urithi wetu, wageni wamepewa nyumba zetu.+   Tumekuwa mayatima, hatuna baba; mama zetu ni kama wajane.+   Ni lazima tulipe ili tunywe maji yetu wenyewe,+ na kuni zetu wenyewe tunazinunua.   Wale wanaotufuatia wamekaribia shingo zetu;Tumechoka, lakini haturuhusiwi kupumzika.+   Tunainyooshea mkono Misri+ na Ashuru,+ ili tupate chakula cha kutosha.*   Mababu zetu waliotenda dhambi hawapo tena, lakini ni lazima tuubebe uovu wao.   Sasa watumishi wanatutawala; hakuna yeyote wa kutunasua kutoka mikononi mwao.   Tunapata chakula chetu* kwa kuhatarisha uhai wetu,*+ kwa sababu ya upanga wa nyikani. 10  Ngozi yetu imekuwa moto kama tanuru, kwa sababu ya makali ya njaa.+ 11  Wamewafedhehesha* wake walio Sayuni, mabikira walio katika majiji ya Yuda.+ 12  Wakuu walitundikwa kwa mikono yao,+ na wazee hawakuheshimiwa.+ 13  Vijana wa kiume wanabeba jiwe la kusagia, na wavulana wanajikwaa kwa sababu ya kubeba mizigo ya kuni. 14  Wazee wametoweka kwenye lango la jiji;+ vijana wa kiume hawapigi muziki wao.+ 15  Shangwe imetoweka mioyoni mwetu; dansi zetu zimegeuka kuwa maombolezo.+ 16  Taji limeanguka kutoka kwenye kichwa chetu. Ole wetu, kwa sababu tumetenda dhambi! 17  Kwa sababu hiyo moyo wetu ni mgonjwa,+Na kwa sababu ya mambo haya macho yetu yamefifia,+ 18  Kwa sababu ya Mlima Sayuni, ambao umeachwa ukiwa;+ sasa mbweha wanatangatanga juu yake. 19  Lakini wewe, Ee Yehova, umeketi kwenye kiti chako cha ufalme milele. Kiti chako kinadumu kizazi baada ya kizazi.+ 20  Kwa nini unatusahau milele na kutuacha kwa muda mrefu sana hivyo?+ 21  Turudishe kwako, Ee Yehova, nasi tutakurudia bila kusita.+ Zifanye siku zetu ziwe mpya kama siku za zamani.+ 22  Hata hivyo, umetukataa kabisa. Unaendelea kutukasirikia vikali sana.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mikate ya kutosha ya kula.”
Tnn., “mikate yetu.”
Au “nafsi zetu.”
Au “Wamewabaka.”