Kulingana na Marko 11:1-33

  • Yesu aingia kwa kishindo (1-11)

  • Mtini walaaniwa (12-14)

  • Yesu asafisha hekalu (15-18)

  • Somo kutoka kwa mtini ulionyauka (19-26)

  • Wataka kujua chanzo cha mamlaka ya Yesu (27-33)

11  Walipokuwa wakikaribia Yerusalemu, Bethfage na Bethania+ kwenye Mlima wa Mizeituni, akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,+  akawaambia: “Nendeni katika kijiji mtakachokiona, na mara tu mtakapoingia mtamwona mwanapunda akiwa amefungwa, ambaye hakuna mtu amewahi kuketi juu yake. Mfungueni na kumleta.  Mtu yeyote akiwauliza, ‘Kwa nini mnamfungua?’ mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa mara moja.’”  Basi wakaenda na kumpata mwanapunda akiwa amefungwa kwenye mlango, karibu na barabara, nao wakamfungua.+  Lakini watu waliokuwa wamesimama hapo wakawauliza: “Kwa nini mnamfungua mwanapunda huyu?”  Wakajibu kama Yesu alivyowaambia, nao wakawaacha waende.  Wakampelekea Yesu huyo mwanapunda,+ wakatandika mavazi yao ya nje juu yake, naye akaketi juu yake.+  Pia, wengi wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani, lakini wengine wakatandaza matawi ya miti waliyokata katika mashamba.+  Watu waliokuwa mbele na wale waliofuata nyuma wakaendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ 10  Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!” 11  Akaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni, akatazama vitu vyote huku na huku, lakini kwa kuwa muda ulikuwa umesonga sana, akaenda Bethania pamoja na wale 12.+ 12  Siku iliyofuata, walipokuwa wakitoka Bethania, akahisi njaa.+ 13  Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda kuona kama angepata chochote. Lakini, alipoufikia, hakupata chochote ila majani, kwa maana hayakuwa majira ya tini. 14  Basi akauambia: “Mtu yeyote asile matunda yako tena kamwe.”+ Nao wanafunzi wake walikuwa wakisikiliza. 15  Wakafika Yerusalemu. Akaingia hekaluni akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, naye akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,+ 16  na hakumruhusu mtu yeyote apite hekaluni akiwa amebeba chombo. 17  Alikuwa akiwafundisha akisema: “Je, haikuandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote’?+ Lakini mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”+ 18  Wakuu wa makuhani na waandishi waliposikia hayo, wakaanza kutafuta njia ya kumuua;+ kwa maana walimwogopa, kwa sababu umati wote ulishangazwa na mafundisho yake.+ 19  Ilipofika jioni, wakatoka jijini. 20  Lakini walipokuwa wakipita asubuhi na mapema, wakaona ule mtini ukiwa umenyauka kuanzia kwenye mizizi.+ 21  Petro, akaukumbuka na kumwambia: “Rabi, ona! ule mtini ulioulaani umenyauka.”+ 22  Yesu akawaambia: “Iweni na imani katika Mungu. 23  Kwa kweli ninawaambia mtu yeyote anayeuambia mlima huu, ‘Ng’oka, ukatupwe baharini,’ bila kuwa na shaka moyoni mwake lakini awe na imani kwamba yale anayosema yatatukia, itakuwa hivyo.+ 24  Ndiyo sababu ninawaambia, mambo yote mnayosali na kuomba, iweni na imani kwamba mmeyapokea, nanyi mtayapata.+ 25  Na mnaposimama kusali, wasameheni watu makosa waliyowatendea; ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu pia.”+ 26 * —— 27  Wakaja tena Yerusalemu. Na alipokuwa akitembea hekaluni, wakuu wa makuhani, waandishi, na wazee wakaja 28  na kumuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Au ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?”+ 29  Yesu akawaambia: “Nitawauliza swali moja. Mkinijibu, nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani. 30  Je, ubatizo wa Yohana+ ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?* Nijibuni.”+ 31  Basi wakaanza kujadiliana kati yao, wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Basi, kwa nini hamkumwamini?’ 32  Lakini je, tutathubutu kusema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’?” Kwa kuwa waliogopa umati, kwa maana umati wote uliamini kwa kweli Yohana alikuwa nabii.+ 33  Basi wakamjibu Yesu: “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia: “Nami siwaambii ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”

Maelezo ya Chini

Au “chanzo chake ni wanadamu?”