Mhubiri 6:1-12

  • Mali bila furaha (1-6)

  • Furahia ulicho nacho (7-12)

6  Kuna msiba mwingine* ambao nimeona chini ya jua, nao ni wa kawaida miongoni mwa wanadamu:  Mungu wa kweli humpa mtu utajiri na mali na utukufu, hivi kwamba hakosi chochote anachotamani;* lakini Mungu wa kweli hamwezeshi kuvifurahia, ingawa mgeni anaweza kuvifurahia. Hili ni ubatili na ni mateso makali.  Mtu akizaa watoto mia moja, aishi miaka mingi na kuzeeka, lakini hafurahii vitu vyake vizuri kabla hajaingia kaburini, sina budi kusema kwamba mtoto aliyefia tumboni ni afadhali kuliko mtu huyo.+  Kwa maana mtoto huyo alikuja bure na kwenda zake gizani, na jina lake limetokomea gizani.  Hata ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye bado ni afadhali* kuliko mtu huyo.+  Kuna faida gani ya kuishi miaka elfu moja mara mbili lakini bila furaha? Je, wote hawaendi mahali palepale?+  Kazi yote ngumu ambayo mtu hufanya ni kwa ajili ya kujaza kinywa chake;+ na bado hamu* yake haitoshelezwi kamwe.  Kwa maana mwenye hekima anamzidi mpumbavu kwa njia gani,+ au maskini hupata faida gani akijua jinsi ya kukabiliana na maisha?*  Ni afadhali mtu afurahie mambo ambayo macho yanaona kuliko kutangatanga akifuatia tamaa zake.* Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo. 10  Chochote ambacho kimekuwapo, tayari kimepewa jina, na mwanadamu anajulikana alivyo; naye hawezi kuzozana na* yule aliye na nguvu zaidi yake. 11  Kadiri maneno* yalivyo mengi, ndivyo ubatili ulivyo mwingi; nayo humnufaishaje mwanadamu? 12  Ni nani anayejua ni jambo gani lililo bora kwa mwanadamu kufanya maishani katika siku chache za maisha yake ya ubatili, anazotumia kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anayeweza kumwambia mwanadamu yatakayotukia chini ya jua baada ya kifo chake?

Maelezo ya Chini

Au “janga lingine.”
Au “hakosi chochote kwa ajili ya nafsi yake.”
Tnn., “ana pumziko zaidi.”
Au “nafsi.”
Tnn., “kutembea mbele ya walio hai.”
Tnn., “kutangatanga kwa nafsi.”
Au “kujitetea mbele ya.”
Au labda, “mambo.”