Nehemia 11:1-36

  • Watu waanza kuishi tena Yerusalemu (1-36)

11  Sasa wakuu wa watu walikuwa wakiishi Yerusalemu;+ lakini watu wengine wote walipiga kura+ ili mtu mmoja kati ya watu kumi aishi Yerusalemu, lile jiji takatifu, na wale wengine tisa waliishi katika majiji mengine.  Isitoshe, watu waliwabariki wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.  Na hawa ndio viongozi wa mkoa* walioishi Yerusalemu. (Waisraeli wengine wote, makuhani, Walawi, watumishi wa hekaluni,*+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ waliishi katika majiji mengine ya Yuda, kila mmoja katika sehemu aliyomiliki jijini.+  Pia, baadhi ya watu wa Yuda na Benjamini waliishi Yerusalemu.) Kati ya watu wa Yuda kulikuwa na Athaya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi,+  na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mshela.  Wana wote wa Perezi walioishi Yerusalemu walikuwa wanaume mashujaa 468.  Hawa ndio waliokuwa watu wa Benjamini: Salu+ mwana wa Meshulamu mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Ithieli mwana wa Yeshaya,  na baada yake Gabai na Salai, watu 928;  na Yoeli mwana wa Zikri alikuwa msimamizi wao, na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa wa pili katika usimamizi wa jiji. 10  Kutoka kwa makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu, Yakini,+ 11  Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli; 12  na ndugu zao waliofanya kazi ya ile nyumba, watu 822; na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya, 13  na ndugu zake, viongozi wa koo,* watu 242, na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemothi mwana wa Imeri, 14  na ndugu zao 128 waliokuwa wanaume hodari na jasiri; na msimamizi wao alikuwa Zabdieli, aliyetoka katika familia mashuhuri. 15  Na kutoka kwa Walawi: Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia mwana wa Buni, 16  na Shabethai+ na Yozabadi,+ wa viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu wa kweli; 17  na Matania,+ mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa waimbaji, aliyeongoza sifa wakati wa sala,+ na Bakbukia, wa pili kati ya ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali mwana wa Yeduthuni.+ 18  Walawi wote katika jiji takatifu walikuwa 284. 19  Na walinzi wa malango walikuwa Akubu, Talmoni,+ na ndugu zao waliolinda malango walikuwa 172. 20  Waisraeli wengine wote, makuhani, na Walawi walikuwa katika majiji mengine yote ya Yuda, kila mmoja katika eneo alilorithi.* 21  Watumishi wa hekaluni*+ walikuwa wakiishi Ofeli,+ nao Siha na Gishpa waliwasimamia watumishi wa hekaluni.* 22  Msimamizi wa Walawi walioishi Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, waimbaji; alisimamia kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli. 23  Kwa maana mfalme alikuwa ametoa amri kwa ajili ya waimbaji,+ na kulikuwa na mpango hususa kuhusu mahitaji yao ya kila siku. 24  Na Pethahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa mshauri wa mfalme* katika kila jambo lililowahusu watu. 25  Kuhusu maeneo na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-arba+ na miji yake, Diboni na miji yake, Yekabzeeli+ na vijiji vyake, 26  huko Yeshua, Molada,+ Beth-peleti,+ 27  Hasar-shuali,+ Beer-sheba na miji yake, 28  Siklagi,+ Mekona na miji yake, 29  En-rimoni,+ Sora,+ na Yarmuthi, 30  Zanoa,+ Adulamu na vijiji vyake, Lakishi+ na mashamba yake, na huko Azeka+ na miji yake. Waliishi* kuanzia Beer-sheba mpaka Bonde la Hinomu.+ 31  Na watu wa Benjamini waliishi Geba,+ Mikmashi, Aiya, Betheli+ na miji yake, 32  Anathothi,+ Nobu,+ Ananiya, 33  Hasori, Rama,+ Gitaimu, 34  Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35  Lodi, na Ono,+ bonde la mafundi. 36  Na baadhi ya vikundi vya Walawi kutoka Yuda waliishi katika eneo la Benjamini.

Maelezo ya Chini

Au “wilaya ya utawala.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Au “hekalu la.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “urithi wake mwenyewe.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Tnn., “alikuwa kwenye mkono wa mfalme.”
Au “Walipiga kambi.”