Nehemia 12:1-47

  • Makuhani na Walawi (1-26)

  • Ukuta wazinduliwa (27-43)

  • Kutegemeza utumishi wa hekalu (44-47)

12  Hawa ndio makuhani na Walawi waliopanda kwenda na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,+ na Yeshua:+ Seraya, Yeremia, Ezra,  Amaria, Maluku, Hatushi,  Shekania, Rehumu, Meremothi,  Ido, Ginethoi, Abiya,  Miyamini, Maadia, Bilga,  Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,  Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hao ndio waliokuwa viongozi wa makuhani na ndugu zao katika siku za Yeshua.  Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli,+ Sherebia, Yuda, na Matania+ aliyeongoza uimbaji wa nyimbo za shukrani akiwa pamoja na ndugu zake.  Walisimama wakitazamana na ndugu zao Bakbukia na Uni wakati wa zamu za kulinda.* 10  Yeshua alimzaa Yoyakimu, Yoyakimu alimzaa Eliashibu,+ naye Eliashibu alimzaa Yoyada.+ 11  Naye Yoyada alimzaa Yonathani, naye Yonathani akamzaa Yadua. 12  Katika siku za Yoyakimu, hawa ndio waliokuwa makuhani, viongozi wa koo:* wa Seraya,+ Meraya; wa Yeremia, Hanania; 13  wa Ezra,+ Meshulamu; wa Amaria, Yehohanani; 14  wa Maluki, Yonathani; wa Shebania, Yosefu; 15  wa Harimu,+ Adna; wa Merayothi, Helkai; 16  wa Ido, Zekaria; wa Ginethoni, Meshulamu; 17  wa Abiya,+ Zikri; wa Miniamini, . . . ;* wa Moadia, Piltai; 18  wa Bilga,+ Shamua; wa Shemaya, Yehonathani; 19  wa Yoyaribu, Matenai; wa Yedaya,+ Uzi; 20  wa Salai, Kalai; wa Amoki, Eberi; 21  wa Hilkia, Hashabia; wa Yedaya, Nethaneli. 22  Viongozi wa koo* za Walawi na za makuhani katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani, na Yadua+ waliandikishwa, vilevile makuhani, mpaka wakati wa ufalme wa Dario Mwajemi. 23  Walawi waliokuwa viongozi wa koo* waliandikishwa katika kitabu cha historia ya nyakati, mpaka siku za Yohanani mwana wa Eliashibu. 24  Viongozi wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua+ mwana wa Kadmieli,+ na ndugu zao walisimama wakitazamana walipokuwa wakiimba sifa na kumshukuru Mungu kulingana na maagizo ya Daudi+ mtu wa Mungu wa kweli, kikundi cha ulinzi kwa kikundi cha ulinzi. 25  Matania,+ Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, na Akubu+ walikuwa walinzi wa malango,+ walilinda maghala yaliyokuwa karibu na malango. 26  Hao walitumikia katika siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua+ mwana wa Yozadaki na katika siku za gavana Nehemia na Ezra+ aliyekuwa kuhani na mwandishi.* 27  Wakati wa kuzindua kuta za Yerusalemu, Walawi walitafutwa kila mahali walipokuwa ili waje Yerusalemu kusherehekea uzinduzi kwa kushangilia, kwa nyimbo za shukrani,+ na kwa matoazi, vinanda, na vinubi. 28  Na wana wa waimbaji* wakakusanyika pamoja kutoka katika wilaya,* kutoka maeneo yaliyokuwa karibu na Yerusalemu, na kutoka vijiji vya Wanetofa,+ 29  kutoka Beth-gilgali,+ na kutoka mashamba ya Geba+ na Azmavethi,+ kwa maana waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu. 30  Na makuhani na Walawi wakajitakasa na kuwatakasa watu,+ malango,+ na ukuta.+ 31  Kisha nikawaleta wakuu wa Yuda juu ya ukuta. Nikapanga makundi mawili makubwa yaliyoimba nyimbo za shukrani na vikundi vya kuwafuata, kikundi kimoja kilienda upande wa kulia wa ukuta kuelekea Lango la Marundo ya Majivu.+ 32  Hoshaya na nusu ya wakuu wa Yuda walitembea nyuma yao, 33  pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 34  Yuda, Benjamini, Shemaya, na Yeremia. 35  Walikuwa pamoja na baadhi ya wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta:+ Zekaria mwana wa Yonathani mwana wa Shemaya mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu,+ 36  na ndugu zake Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, na Hanani, wakiwa na vyombo vya muziki vya Daudi+ mtu wa Mungu wa kweli; na Ezra+ mwandishi* akawatangulia. 37  Kwenye Lango la Chemchemi+ walipanda moja kwa moja Ngazi+ ya Jiji la Daudi+ kupitia njia inayopanda kwenye ukuta juu ya Nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji+ upande wa mashariki. 38  Kundi la pili lililoimba nyimbo za shukrani lilitembea kuelekea kushoto,* nami nikalifuata pamoja na nusu ya watu, juu ya ukuta kwenye Mnara wa Majiko ya Kuokea+ mpaka kwenye Ukuta Mpana+ 39  na kupita juu ya Lango la Efraimu+ na juu ya Lango la Jiji la Kale+ mpaka kwenye Lango la Samaki,+ Mnara wa Hananeli,+ Mnara wa Mea, na mpaka kwenye Lango la Kondoo;+ kisha wakasimama kwenye Lango la Mlinzi. 40  Mwishowe yale makundi mawili yaliyoimba nyimbo za shukrani yakasimama mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli; mimi pia nikasimama pamoja na nusu ya watawala wasaidizi waliokuwa pamoja nami, 41  na makuhani Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania, wakiwa na tarumbeta, 42  na Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, na Ezeri. Na waimbaji hao wakaimba kwa sauti kubwa wakiongozwa na Izrahia. 43  Siku hiyo walitoa dhabihu nyingi na kushangilia,+ kwa maana Mungu wa kweli aliwafanya washangilie kwa shangwe kubwa. Wanawake na watoto wakashangilia pia,+ hivi kwamba sauti za kushangilia jijini Yerusalemu zikasikika mbali sana.+ 44  Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia maghala+ ya michango,+ mazao ya kwanza,+ na sehemu za kumi.+ Kutoka katika mashamba ya majiji walipaswa kukusanya kwenye maghala hayo mafungu yaliyoamriwa na Sheria+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa na shangwe huko Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi waliokuwa wakihudumu. 45  Nao wakaanza kushughulikia majukumu waliyopewa na Mungu wao na kutimiza wajibu wa kutakasa, kama walivyofanya waimbaji na walinzi wa malango, kulingana na maagizo ya Daudi na ya Sulemani mwanawe. 46  Kwa maana zamani za kale katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na viongozi wa* waimbaji wa nyimbo za kumsifu na kumshukuru Mungu.+ 47  Na katika siku za Zerubabeli+ na siku za Nehemia, Waisraeli wote walitoa mafungu kwa ajili ya waimbaji+ na walinzi wa malango,+ kulingana na uhitaji wa kila siku. Pia, waliweka kando fungu kwa ajili ya Walawi,+ na Walawi waliweka kando fungu kwa ajili ya wazao wa Haruni.

Maelezo ya Chini

Au labda, “wakati wa utumishi.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Inaonekana jina fulani limeondolewa hapa katika maandishi ya Kiebrania.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “aliyenakili maandishi.”
Au “Na waimbaji waliozoezwa.”
Yaani, wilaya iliyozunguka Yordani.
Au “aliyenakili maandishi.”
Au “lilitembea mbele.”
Tnn., “vichwa vya.”