Yoshua 10:1-43

  • Waisraeli wawatetea Wagibeoni (1-7)

  • Yehova awapigania Waisraeli (8-15)

    • Mawe yawaangukia maadui wanaokimbia (11)

    • Jua lasimama tuli (12-14)

  • Wafalme watano wa maadui wauawa (16-28)

  • Majiji ya kusini yatekwa (29-43)

10  Mara tu Mfalme Adoni-sedeki wa Yerusalemu aliposikia kwamba Yoshua ameteka Ai na kuliangamiza, na kulitendea Ai na mfalme wake+ kama alivyolitendea Yeriko na mfalme wake,+ na jinsi wakaaji wa Gibeoni walivyofanya amani na Waisraeli+ na kuendelea kukaa kati yao,  akaogopa sana,+ kwa sababu Gibeoni lilikuwa jiji kubwa kama majiji yaliyotawaliwa na mfalme. Lilikuwa kubwa kuliko Ai,+ na wanaume wake wote walikuwa mashujaa.  Basi Adoni-sedeki mfalme wa Yerusalemu akatuma ujumbe huu kwa Hohamu mfalme wa Hebroni,+ Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na kwa Debiri mfalme wa Egloni:+  “Njooni mnisaidie kuwashambulia wakaaji wa Gibeoni, kwa sababu wamefanya amani na Yoshua na Waisraeli.”+  Ndipo wafalme watano wa Waamori,+ yaani, mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Hebroni, mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni wakakusanyika pamoja na majeshi yao, wakaenda kupiga kambi ili kulishambulia jiji la Gibeoni.  Kisha wazee wa Gibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kambini Gilgali,+ wakisema: “Usituache* sisi watumwa wako.+ Njoo haraka ili utuokoe na kutusaidia! Wafalme wote wa Waamori kutoka katika eneo lenye milima wamekusanyika ili kutushambulia.”  Basi Yoshua akapanda kutoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote na mashujaa hodari.+  Ndipo Yehova akamwambia Yoshua: “Usiwaogope,+ kwa maana nimewatia mikononi mwako.+ Hakuna mtu yeyote kati yao atakayekushinda.”+  Yoshua akawashambulia ghafla baada ya kutembea usiku kucha kutoka Gilgali. 10  Yehova akawavuruga,+ na Waisraeli wakawaangamiza wengi wao kule Gibeoni, wakawafuatia kwenye njia inayopanda kwenda Beth-horoni na kuwaua mpaka Azeka na Makeda. 11  Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli, Yehova akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka angani kwenye mteremko wa Beth-horoni mpaka Azeka, nao wakafa. Kwa kweli, wale waliouawa na mvua ya mawe walikuwa wengi kuliko wale waliouawa na Waisraeli kwa upanga. 12  Ni siku hiyo, siku ambayo Yehova aliwashinda kabisa Waamori mbele ya Waisraeli, ndipo Yoshua alipomwambia hivi Yehova mbele ya Waisraeli: “Jua, simama tuli+ juu ya Gibeoni,+Na mwezi, juu ya Bonde la* Aiyaloni.” 13  Basi jua likasimama tuli na mwezi ukatulia mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi dhidi ya maadui wake. Je, haijaandikwa hivi katika kitabu cha Yashari:+ Jua lilisimama tuli katikati ya mbingu na halikutua kwa siku nzima? 14  Haijawahi kamwe kutokea siku kama hiyo, kabla au baada yake, ambayo Yehova aliisikiliza sauti ya mwanadamu+ katika njia hiyo, kwa sababu Yehova alikuwa akiwapigania Waisraeli.+ 15  Baada ya mambo hayo Yoshua na Waisraeli wote wakarudi kambini Gilgali.+ 16  Wakati huo, wale wafalme watano walikimbia na kujificha pangoni kule Makeda.+ 17  Yoshua akaambiwa: “Wale wafalme watano wamejificha pangoni kule Makeda.”+ 18  Basi Yoshua akasema: “Bingirisheni mawe makubwa kwenye mwingilio wa pango hilo na kuweka walinzi hapo. 19  Lakini ninyi wengine msikae hapo. Wakimbizeni maadui wenu na kuwashambulia kutokea nyuma.+ Msiwape nafasi ya kuingia katika majiji yao, kwa kuwa Yehova Mungu wenu amewatia mikononi mwenu.” 20  Baada ya Yoshua na Waisraeli kuwaangamiza karibu watu wote na wachache waliobaki kukimbilia katika majiji yenye ngome, 21  Waisraeli wote wakarudi salama kambini kwa Yoshua kule Makeda. Hakuna mtu aliyethubutu kusema neno lolote* dhidi ya Waisraeli. 22  Kisha Yoshua akasema, “Fungueni mwingilio wa pango, watoeni nje wale wafalme watano na kuwaleta kwangu.” 23  Basi wakawatoa pangoni wafalme hawa watano na kuwaleta kwake: mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Hebroni, mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni.+ 24  Walipomletea Yoshua wafalme hao, akawaita wanaume wote wa Israeli na kuwaambia makamanda wa jeshi walioenda naye: “Njooni. Wakanyageni nyuma ya shingo wafalme hawa.” Basi wakaja na kuwakanyaga nyuma ya shingo.+ 25  Ndipo Yoshua akawaambia: “Msiogope wala msihofu.+ Iweni jasiri na imara, kwa maana hivi ndivyo Yehova atakavyowatendea maadui wenu wote ambao mnapigana nao.”+ 26  Kisha Yoshua akawapiga na kuwaua, akawatundika juu ya miti mitano, wakaning’inia juu ya miti hiyo mpaka jioni. 27  Na jua lilipotua, Yoshua akaagiza washushwe kutoka kwenye miti+ hiyo na kutupwa ndani ya pango ambamo walikuwa wamejificha. Kisha mawe makubwa yakawekwa kwenye mwingilio wa pango hilo, nayo yapo mpaka leo. 28  Yoshua akateka jiji la Makeda+ siku hiyo na kuwaangamiza wakaaji wake kwa upanga. Akamwangamiza mfalme wake na wakaaji wote, na hakuna mtu yeyote aliyebaki.*+ Alimtendea mfalme wa Makeda+ kama alivyomtendea mfalme wa Yeriko. 29  Kisha Yoshua na Waisraeli wote wakatoka Makeda na kwenda Libna, wakalishambulia jiji la Libna.+ 30  Yehova akalitia pia jiji hilo na mfalme wake+ mikononi mwa Waisraeli, wakalishambulia na kuwaangamiza wakaaji wote kwa upanga, na hakuna yeyote aliyebaki humo. Wakamtendea mfalme wake kama walivyomtendea mfalme wa Yeriko.+ 31  Kisha Yoshua na Waisraeli wote wakatoka Libna na kwenda Lakishi,+ wakapiga kambi huko na kulishambulia. 32  Yehova akalitia jiji la Lakishi mikononi mwa Waisraeli, nao wakaliteka siku ya pili. Wakalishambulia na kuwaangamiza wakaaji wote* kwa upanga,+ kama walivyofanya kule Libna. 33  Ndipo Horamu mfalme wa Gezeri+ akaenda kulisaidia Lakishi, lakini Yoshua akamuua yeye na watu wake wote, na hakuna yeyote aliyebaki. 34  Kutoka Lakishi, Yoshua na Waisraeli wote wakaenda Egloni,+ wakapiga kambi huko na kulishambulia. 35  Wakaliteka siku hiyo na kuliangamiza kwa upanga. Wakawaangamiza wakaaji wote siku hiyo, kama walivyofanya kule Lakishi.+ 36  Kutoka Egloni, Yoshua na Waisraeli wote wakaenda Hebroni+ na kulishambulia. 37  Wakaliteka na kuliangamiza kwa upanga jiji hilo, mfalme wake, miji yake, na wakaaji wote, na hakuna yeyote aliyebaki. Yoshua aliliangamiza pamoja na wakaaji wote,* kama alivyofanya kule Egloni. 38  Mwishowe Yoshua na Waisraeli wote wakaelekea Debiri+ na kulishambulia. 39  Akaliteka pamoja na mfalme wake, na miji yake yote, wakawaangamiza wakaaji wote kwa upanga,+ na hakuna yeyote aliyebaki.+ Alilitendea Debiri na mfalme wake kama alivyolitendea Hebroni na pia Libna na mfalme wake. 40  Hivyo Yoshua akaiteka nchi yote kutia ndani eneo lenye milima, Negebu, Shefela,+ na miteremko, na kuwashinda wafalme wao wote, na hakuna yeyote aliyebaki; alimwangamiza kila kiumbe anayepumua,+ kama Yehova Mungu wa Israeli alivyoamuru.+ 41  Yoshua aliwashinda kuanzia Kadesh-barnea+ mpaka Gaza+ na nchi yote ya Gosheni+ kufika Gibeoni.+ 42  Yoshua aliwateka wafalme hao wote na nchi zao kwa wakati mmoja, kwa sababu Yehova Mungu wa Israeli alikuwa akiwapigania Waisraeli.+ 43  Hatimaye Yoshua na Waisraeli wote wakarudi kambini Gilgali.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Usiulegeze mkono wako kutuelekea.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Tnn., “kunoa ulimi wake.”
Au “nafsi yoyote iliyobaki.”
Tnn., “nafsi zote.”
Au “kila nafsi.”