Yoshua 14:1-15

  • Kugawanywa kwa maeneo magharibi mwa Yordani (1-5)

  • Kalebu arithi Hebroni (6-15)

14  Basi huu ndio urithi ambao kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo* za makabila ya Israeli waliwapa Waisraeli katika nchi ya Kanaani.+  Waligawiwa urithi wao kwa kura,+ kama Yehova alivyomwagiza Musa ayagawie yale makabila tisa na nusu.+  Musa alikuwa tayari ameyapa makabila mawili na nusu urithi ng’ambo ya* Yordani,+ lakini hakuwapa Walawi urithi kati yao.+  Wazao wa Yosefu walihesabiwa kuwa makabila mawili,+ Manase na Efraimu;+ nao hawakuwagawia Walawi urithi nchini, isipokuwa majiji+ ya kuishi na malisho kwa ajili ya mifugo yao na mali zao.+  Basi, Waisraeli waliigawanya nchi kama Yehova alivyomwamuru Musa.  Ndipo watu wa kabila la Yuda wakaenda kwa Yoshua kule Gilgali,+ na Kalebu+ mwana wa Yefune Mkenizi akamwambia: “Unajua vizuri maneno ambayo Yehova alimwambia Musa+ mtumishi wa Mungu wa kweli+ juu yangu na juu yako kule Kadesh-barnea.+  Nilikuwa na umri wa miaka 40 Musa mtumishi wa Yehova aliponituma kutoka Kadesh-barnea kwenda kuipeleleza nchi,+ nami nikamletea habari ya kweli.*+  Ingawa ndugu zangu walioenda pamoja nami waliwavunja watu moyo,* mimi nilimfuata Yehova Mungu wangu kwa moyo wote.*+  Siku hiyo, Musa aliapa hivi: ‘Nchi ambayo mguu wako umekanyaga itakuwa urithi wako na wa wana wako milele, kwa sababu umemfuata Yehova Mungu wangu kwa moyo wote.’+ 10  Basi kama alivyoahidi,+ Yehova amenihifadhi hai+ kwa miaka 45 tangu Yehova alipompa Musa ahadi hiyo Waisraeli walipotembea nyikani;+ ningali hai leo, nina umri wa miaka 85. 11  Lakini bado nina nguvu nilizokuwa nazo siku ambayo Musa alinituma. Bado nina nguvu nilizokuwa nazo wakati huo za kupigana vitani na kufanya kazi nyingine. 12  Kwa hiyo, nipe eneo hili lenye milima ambalo Yehova aliahidi siku hiyo. Ingawa ulisikia siku hiyo kwamba kuna Waanaki+ wanaoishi huko katika majiji makubwa yenye ngome,+ bila shaka* Yehova atakuwa pamoja nami,+ nami nitawafukuza,* kama Yehova alivyoahidi.”+ 13  Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune na kumpa Hebroni kuwa urithi wake.+ 14  Ndiyo sababu Hebroni limekuwa urithi wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi mpaka leo, kwa sababu alimfuata Yehova Mungu wa Israeli kwa moyo wote.+ 15  Hapo awali Hebroni liliitwa Kiriath-arba+ (Arba alikuwa mtu maarufu miongoni mwa Waanaki). Nchi ikawa na amani bila vita.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, upande wa mashariki wa.
Tnn., “neno kama lilivyokuwa moyoni mwangu.”
Tnn., “waliifanya mioyo ya watu iyeyuke.”
Tnn., “kikamilifu; kabisa.”
Au “nitachukua nchi yao.”
Au “inaelekea.”