Yoshua 19:1-51

  • Urithi wa kabila la Simeoni (1-9)

  • Urithi wa kabila la Zabuloni (10-16)

  • Urithi wa kabila la Isakari (17-23)

  • Urithi wa kabila la Asheri (24-31)

  • Urithi wa kabila la Naftali (32-39)

  • Urithi wa kabila la Dani (40-48)

  • Urithi wa Yoshua (49-51)

19  Kura ya pili+ ilikuwa ya Simeoni, kwa ajili ya kabila la Simeoni+ kulingana na koo zao. Nao walipewa urithi kati ya urithi wa kabila la Yuda.+  Urithi wao ulikuwa Beer-sheba,+ Sheba, Molada,+  Hasar-shuali,+ Bala, Esemu,+  Eltoladi,+ Bethuli, Horma,  Siklagi,+ Beth-markabothi, Hasar-susa,  Beth-lebaothi,+ na Sharuheni—majiji 13 na vijiji vyake;  Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani+—majiji manne na vijiji vyake;  na vijiji vyote vilivyozunguka majiji hayo mpaka Baalath-beeri, Rama ya kusini. Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Simeoni kulingana na koo zao.  Kabila la Yuda lilikuwa na eneo kubwa sana, basi wazao wa Simeoni waligawiwa sehemu ya eneo hilo. Hivyo wazao wa Simeoni walipata urithi katikati ya kabila la Yuda.+ 10  Kura ya tatu+ ilikuwa ya wazao wa Zabuloni+ kulingana na koo zao, na mpaka wa urithi wao ulifika Saridi. 11  Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Mareali kufika Dabeshethi na kuingia bondeni* mbele ya Yokneamu. 12  Na kutoka Saridi, ulielekea upande wa mashariki, na kufika kwenye mpaka wa Kisloth-tabori na kuendelea hadi Daberathi+ na kupanda hadi Yafia. 13  Kisha ukaelekea mashariki hadi Gath-heferi+ na kufika Eth-kazini, hadi Rimoni, na kufika Nea. 14  Na mpaka huo uligeuka kuelekea Hanathoni upande wa kaskazini, na kufika kwenye Bonde la Iftah-eli, 15  na Katathi, Nahalali, Shimroni,+ Idala, na Bethlehemu+—majiji 12 na vijiji vyake. 16  Huo ndio uliokuwa urithi wa wazao wa Zabuloni kulingana na koo zao.+ Hayo ndiyo yaliyokuwa majiji na vijiji vyake. 17  Kura ya nne+ ilikuwa ya Isakari,+ kwa ajili ya wazao wa Isakari kulingana na koo zao. 18  Na mpaka wao ulifika Yezreeli,+ Kesulothi, Shunemu,+ 19  Hafaraimu, Shioni, Anaharathi, 20  Rabithi, Kishioni, Ebesi, 21  Remethi, En-ganimu,+ En-hada, na Beth-pasesi. 22  Na mpaka huo ulifika Tabori+ na Shahasuma na Beth-shemeshi, na kufika kwenye Mto Yordani—majiji 16 na vijiji vyake. 23  Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Isakari kulingana na koo zao,+ majiji na vijiji vyake. 24  Kura ya tano+ ilikuwa ya kabila la Asheri+ kulingana na koo zao. 25  Mpaka wao ulipita Helkathi,+ Hali, Beteni, Akshafi, 26  Alameleki, Amadi, na Mishali. Nao ulifika upande wa magharibi hadi Karmeli+ na kuelekea Shihor-libnathi, 27  nao uligeuka na kuelekea Beth-dagoni upande wa mashariki na kufika Zabuloni na Bonde la Iftah-eli upande wa kaskazini, hadi Beth-emeki na Neieli, kisha ukaelekea Kabuli upande wa kushoto, 28  na Ebroni, Rehobu, Hamoni, na Kana hadi Sidoni Kuu.+ 29  Na mpaka huo ukageuka kurudi Rama na kufika kwenye jiji la Tiro lenye ngome.+ Kisha ukageuka kurudi Hosa, na kufika kwenye bahari katika eneo la Akzibu, 30  Uma, Afeki,+ na Rehobu+—majiji 22 na vijiji vyake. 31  Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Asheri kulingana na koo zao.+ Hayo ndiyo yaliyokuwa majiji na vijiji vyake. 32  Kura ya sita+ ilikuwa ya wazao wa Naftali, kwa ajili ya wazao wa Naftali kulingana na koo zao. 33  Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka kwenye mti mkubwa kule Saananimu,+ kuelekea Adami-nekebu na Yabneeli hadi Lakumu; na kufika kwenye Mto Yordani. 34  Na kutoka huko ukageuka na kuelekea magharibi hadi Aznoth-tabori na kwenda Hukkoki mpaka Zabuloni upande wa kusini na kupakana na Asheri upande wa magharibi na kuendelea hadi Yuda, na kufika kwenye Mto Yordani upande wa mashariki. 35  Na majiji yenye ngome yalikuwa Sidimu, Seri, Hamathi,+ Rakathi, Kinerethi, 36  Adama, Rama, Hasori,+ 37  Kedeshi,+ Edrei, En-hasori, 38  Yironi, Migdal-eli, Horemu, Beth-anathi, na Beth-shemeshi+—majiji 19 na vijiji vyake. 39  Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Naftali kulingana na koo zao,+ majiji na vijiji vyake. 40  Kura ya saba+ ilikuwa ya kabila la Dani+ kulingana na koo zao. 41  Na mpaka wa urithi wao ulipita Sora,+ Eshtaoli, Ir-shemeshi, 42  Shaalabini,+ Aiyaloni,+ Ithla, 43  Eloni, Timna,+ Ekroni,+ 44  Elteke, Gibethoni,+ Baalathi, 45  Yehudi, Bene-beraki, Gath-rimoni,+ 46  Me-yarkoni, na Rakoni, mpaka ukiwa mbele ya Yopa.+ 47  Lakini eneo la kabila la Dani halikuwatosha kwa sababu lilikuwa dogo.+ Basi wakaenda kushambulia jiji la Leshemu,+ wakaliteka na kuwaangamiza wakaaji wake kwa upanga. Wakalimiliki na kukaa ndani yake, kisha wakabadili jina Leshemu kuwa Dani, jina la babu yao.+ 48  Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Dani kulingana na koo zao. Hayo ndiyo yaliyokuwa majiji na vijiji vyake. 49  Basi wakamaliza kugawanya nchi ya urithi kulingana na maeneo yake. Kisha Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi kati yao. 50  Kwa agizo la Yehova walimpa jiji ambalo aliomba, yaani, Timnath-sera,+ katika eneo lenye milima la Efraimu, akalijenga upya na kukaa ndani yake. 51  Huo ndio urithi ambao kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo* za makabila ya Waisraeli waligawanya+ kwa kura kule Shilo+ mbele za Yehova, kwenye mlango wa hema la mkutano.+ Basi wakamaliza kuigawanya nchi.

Maelezo ya Chini

Au “korongoni.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.