Zekaria 10:1-12

  • Mwombeni Yehova awape mvua, msiombe miungu ya uwongo (1, 2)

  • Yehova awaunganisha watu wake (3-12)

    • Kiongozi kutoka katika nyumba ya Yuda (3, 4)

10  “Mwombeni Yehova mvua wakati wa mvua ya masika. Yehova ndiye anayetengeneza mawingu ya dhoruba,Ndiye anayewaletea mvua,+Na kumpa kila mtu mimea ya shambani.   Kwa maana sanamu za terafimu* zimesema uwongo;*Na wabashiri* wameona maono ya uwongo. Husimulia ndoto zisizo na faida,Na kwa ubatili wao hujaribu kufariji. Ndiyo sababu watatangatanga kama kondoo. Watateseka, kwa maana hakuna mchungaji.   Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji,Nitawaadhibu viongozi* wanaowakandamiza watu;Kwa maana Yehova wa majeshi amelielekezea uangalifu kundi lake,+ ameielekezea uangalifu nyumba ya Yuda,Naye amewafanya wawe kama farasi wake mwenye fahari vitani.   Mtu mkuu anatoka kwake,*Mtawala anayemtegemeza anatoka kwake,*Upinde wa vita unatoka kwake;Na kila mwangalizi* hutoka kwake, wote pamoja.   Nao watakuwa kama mashujaa,Wanaokanyaga matope barabarani wakiwa vitani. Watapigana vita, kwa maana Yehova yupo pamoja nao;+Na wapanda farasi wataaibishwa.+   Nitaifanya nyumba ya Yuda iwe kuu sana,Nami nitaiokoa nyumba ya Yosefu.+ Nitawarudisha,Kwa maana nitawaonyesha rehema;+Nao watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwatupa;+Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, nami nitawajibu.   Ni lazima watu wa Efraimu wawe kama shujaa hodari,Na moyo wao utashangilia kana kwamba wamekunywa divai.+ Wana wao wataona jambo hilo na kushangilia;Moyo wao utashangilia katika Yehova.+   ‘Nitawapigia mluzi na kuwakusanya pamoja;Kwa maana nitawakomboa,+ nao watakuwa wengi,Na kuendelea kuongezeka.   Ingawa ninawatawanya kama mbegu miongoni mwa mataifa,Watanikumbuka wakiwa katika maeneo ya mbali;Watahuishwa na kurudi pamoja na wana wao. 10  Nitawarudisha kutoka nchini MisriNa kuwakusanya kutoka Ashuru;+Nitawaleta katika nchi ya Gileadi+ na Lebanoni,Na hakutakuwa na nafasi zaidi ya kuwatosha.+ 11  Ni lazima apite baharini kwa msukosuko;Na humo baharini atayapiga mawimbi yatulie;+Vilindi vyote vya Mto Nile vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa,Na fimbo ya mfalme wa Misri itaondoka.+ 12  Nitawafanya wawe wakuu sana katika jina langu Yehova,+Nao watatembea huku na kule katika jina langu,’+ asema Yehova.”

Maelezo ya Chini

Au “miungu ya familia; sanamu.”
Au “zimesema mambo ya uchawi; mazingaombwe.”
Au “waaguzi.”
Tnn., “mabeberu.”
Tnn., “Mnara wa pembeni unatoka kwake,” unafananisha mtu muhimu au wa maana sana; kiongozi.
Tnn., “Kigingi kinatoka kwake,” kinafananisha mtegemezaji; mtawala.”
Au “msimamizi wa watumwa.”