Zekaria 11:1-17

  • Madhara ya kumkataa mchungaji wa kweli aliyetumwa na Mungu (1-17)

    • “Lichunge kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa” (4)

    • Fimbo mbili: Uzuri na Muungano (7)

    • Mshahara wa mchungaji: vipande 30 vya fedha (12)

    • Fedha hizo zatupwa kwenye hazina (13)

11  “Fungua milango yako, Ee Lebanoni,Ili moto uteketeze mierezi yako.   Omboleza kwa sauti, ewe mberoshi, kwa maana mwerezi umeanguka;Miti mikubwa imeharibiwa! Ombolezeni kwa sauti, enyi mialoni ya Bashani,Kwa maana msitu mnene umefyekwa!   Sikilizeni! Maombolezo ya wachungaji,Kwa maana fahari yao imeharibiwa. Sikilizeni! Mingurumo ya wanasimba,*Kwa maana mapori makubwa yaliyo kwenye kingo za Yordani yameharibiwa.  “Yehova Mungu wangu anasema hivi: ‘Lichunge kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa,+  ambao wanachinjwa na wanunuzi wao+ lakini wanunuzi hao hawahesabiwi kuwa na hatia. Na wale wanaowauza+ husema, “Yehova na asifiwe, kwa maana nitakuwa tajiri.” Na wachungaji wao hawawahurumii.’+  “‘Kwa maana sitawahurumia tena wakaaji wa nchi,’ asema Yehova. ‘Kwa hiyo nitamtia kila mtu mikononi mwa jirani yake na mfalme wake; nao wataipondaponda nchi, nami sitawaokoa kutoka mikononi mwao.’”  Nami nikaanza kulichunga kundi la kondoo wanaopaswa kuchinjwa,+ kwa faida yenu, enyi kondoo mnaoteseka. Kwa hiyo nikachukua fimbo mbili, moja nikaiita Uzuri, na nyingine Muungano,+ nikaanza kulichunga kundi hilo la kondoo.⁠  Nami nikawafukuza wachungaji watatu katika mwezi mmoja, kwa maana nilichoshwa nao, nao pia wakachukizwa nami.  Kisha nikasema: “Sitaendelea kuwachunga ninyi. Yule anayekufa na afe, na yule anayeangamia na aangamie. Na wale wanaobaki, kila mmoja wao amle mwenzake.” 10  Basi nikachukua fimbo yangu inayoitwa Uzuri+ na kuikatakata, na hivyo nikavunja agano langu nililokuwa nimefanya na mataifa yote. 11  Basi likavunjika siku hiyo, na kondoo walioteseka waliokuwa wakinitazama walijua kwamba hilo lilikuwa neno la Yehova. 12  Kisha nikawaambia: “Ikiwa mnaona ni vema, nipeni mshahara wangu; kama sivyo, msinipe.” Basi wakanilipa* mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.+ 13  Ndipo Yehova akaniambia: “Vitupe katika hazina—thamani kubwa waliyonikadiria.”+ Kwa hiyo nikavichukua vipande hivyo 30 vya fedha na kuvitupa katika hazina ya nyumba ya Yehova.+ 14  Kisha nikaikatakata fimbo yangu ya pili, inayoitwa Muungano,+ na hivyo nikauvunja undugu kati ya Yuda na Israeli.+ 15  Na Yehova akaniambia: “Sasa vichukue vifaa vya mchungaji asiyefaa.+ 16  Kwa maana ninamruhusu mchungaji ainuke nchini. Hatawatunza kondoo wanaoangamia;+ hatawatafuta walio wachanga au kuwaponya waliojeruhiwa+ au kuwalisha wanaoweza kusimama. Badala yake, atamla kondoo aliyenona+ na kuwang’oa kwato kondoo.+ 17  Ole wake mchungaji wangu asiyefaa,+ anayeliacha kundi!+ Upanga utakata mkono wake na jicho lake la kulia. Mkono wake utapooza kabisa,Na jicho lake la kulia litapofuka* kabisa.”

Maelezo ya Chini

Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Tnn., “wakanipimia.”
Tnn., “litafifia.”