Zekaria 8:1-23

  • Yehova aleta amani na ukweli Sayuni (1-23)

    • Yerusalemu, “jiji la ukweli” (3)

    • “Kila mtu amwambie mwenzake ukweli” (16)

    • Siku za kufunga zitakuwa siku za sherehe (18, 19)

    • ‘Twendeni kwa bidii kumtafuta Yehova’ (21)

    • Watu kumi watashika joho la Myahudi (23)

8  Neno la Yehova wa majeshi lilinijia tena, likisema:  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Nitakuwa na bidii kwa ajili ya Sayuni, bidii nyingi,+ na kwa hasira kali nitakuwa na bidii kwa ajili yake.’”  “Yehova anasema hivi: ‘Nitarudi Sayuni+ na kukaa Yerusalemu;+ na Yerusalemu litaitwa jiji la ukweli,*+ na mlima wa Yehova wa majeshi utaitwa mlima mtakatifu.’”+  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Wanaume wazee na wanawake wazee wataketi tena katika viwanja vya jiji la Yerusalemu, kila mmoja wao akiwa na mkongojo wake mkononi kwa sababu ya umri wake mkubwa.*+  Na viwanja vya jiji vitajaa wavulana na wasichana wanaocheza.’”+  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Ingawa jambo hilo huenda likaonekana kuwa gumu kwa watu wa taifa hili watakaobaki siku hizo, je, linaweza kuwa gumu sana machoni pangu pia?’ asema Yehova wa majeshi.”  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Tazama, ninawaokoa watu wangu kutoka katika nchi ya mashariki na nchi ya magharibi.*+  Nami nitawaleta ndani, nao wataishi Yerusalemu;+ watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao+ katika ukweli* na katika uadilifu.’”  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Mikono yenu na iwe na nguvu,*+ ninyi ambao sasa mnasikia maneno haya yanayotoka katika kinywa cha manabii,+ maneno yaleyale yaliyosemwa siku ambayo msingi wa nyumba ya Yehova wa majeshi uliwekwa ili hekalu lijengwe. 10  Kwa maana kabla ya wakati huo, mshahara haukulipwa kwa ajili ya mwanadamu wala kwa ajili ya mnyama;+ na haikuwa salama kuingia wala kutoka kwa sababu ya maadui, kwa maana nilisababisha uadui kati ya watu wote.’ 11  “‘Lakini sasa sitawatendea watu waliobaki wa taifa hili kama nilivyowatendea zamani,’+ asema Yehova wa majeshi. 12  ‘Kwa maana mbegu ya amani itapandwa; mzabibu utazaa matunda yake na dunia itatoa mazao yake,+ na mbingu zitatoa umande wake; nami nitawapa watu waliobaki wa taifa hili vitu hivi vyote viwe urithi wao.+ 13  Na kama mlivyokuwa kitu cha kulaaniwa miongoni mwa mataifa,+ Ee nyumba ya Yuda na nyumba ya Israeli, vivyo hivyo nitawaokoa, nanyi mtakuwa baraka.+ Msiogope!+ Mikono yenu na iwe na nguvu.’*+ 14  “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘“Kama nilivyokusudia kuwaletea msiba kwa sababu mababu zenu walinikasirisha,” asema Yehova wa majeshi, “nami sikughairi,+ 15  ndivyo nilivyokusudia sasa kulitendea mema jiji la Yerusalemu na nyumba ya Yuda.+ Msiogope!”’+ 16  “‘Haya ndiyo mambo mnayopaswa kufanya: Kila mtu amwambie mwenzake ukweli,+ na hukumu mnazotoa katika malango yenu zinapaswa kutetea ukweli na amani.+ 17  Msipangiane njama za msiba mioyoni mwenu,+ nanyi msipende kiapo chochote cha uwongo;+ kwa maana hayo yote ni mambo ninayochukia,’+ asema Yehova.” 18  Neno la Yehova wa majeshi lilinijia tena, likisema: 19  Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Mfungo wa mwezi wa nne,+ mfungo wa mwezi wa tano,+ mfungo wa mwezi wa saba,+ na mfungo wa mwezi wa kumi+ zitakuwa pindi za shangwe na kushangilia kwa ajili ya nyumba ya Yuda—sherehe za kushangilia.+ Kwa hiyo pendeni ukweli na amani.’ 20  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Itatukia kwamba mataifa na wakaaji wa majiji mengi watakuja; 21  na wakaaji wa jiji moja wataenda kwa wakaaji wa jiji lingine na kuwaambia: “Twendeni kwa bidii tukamsihi Yehova atupe kibali chake* na kumtafuta Yehova wa majeshi. Mimi pia nitaenda.”+ 22  Na mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja Yerusalemu kumtafuta Yehova wa majeshi + na kumsihi Yehova awape kibali chake.’* 23  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Siku hizo watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa+ watashika, naam, watashika kwa nguvu joho* la Myahudi,* wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi,+ kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”’”+

Maelezo ya Chini

Au “uaminifu.”
Tnn., “kwa sababu ya wingi wa siku.”
Au “nchi ya mawio ya jua na nchi ya machweo ya jua.”
Au “uaminifu.”
Au “Iweni jasiri.”
Au “Iweni jasiri.”
Tnn., “tukautulize uso wa Yehova.”
Tnn., “kuutuliza uso wa Yehova.”
Au “upindo wa vazi.”
Tnn., “mwanamume Myahudi.”