Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 87-91

Kaa Mahali pa Siri pa Aliye Juu Zaidi

Kaa Mahali pa Siri pa Aliye Juu Zaidi

Tunapata ulinzi wa kiroho katika “mahali pa siri” pa Yehova

91:1, 2, 9-14

  • Leo, ili tukae katika “mahali pa siri” pa Yehova ni lazima tujiweke wakfu na kubatizwa

  • Mahali hapo pa siri hapatambuliwi na wale ambao hawamtegemei Mungu

  • Wale walio mahali pa siri pa Yehova hawaathiriwi na mtu yeyote au kitu chochote kinachoweza kuhatarisha imani na upendo wao kwa Mungu

“Mwindaji wa ndege” anajaribu kutunasa

91:3

  • Ndege ni viumbe wanaojihadhari sana na wasionaswa kwa urahisi

  • Wawindaji huchunguza tabia za ndege kwa uangalifu na kisha kutafuta njia za kuwanasa

  • Shetani, “mwindaji wa ndege,” huwachunguza watu wa Yehova na kuweka mitego iliyokusudiwa kuharibu uhusiano wao na Yehova

Mitego minne hatari inayotumiwa na Shetani:

  • Kuwaogopa Wanadamu

  • Kupenda Vitu vya Kimwili

  • Burudani Zisizofaa

  • Tofauti za Kibinafsi