Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | AYUBU 33-37

Rafiki wa Kweli Anatoa Shauri Lenye Kujenga

Rafiki wa Kweli Anatoa Shauri Lenye Kujenga

Elihu alipoanza kuongea, ushauri wake ulikuwa tofauti kabisa na ule wa Elifazi, Bildadi, na Sofari.Alizungumzia mambo tofauti na pia alimtendea Ayubu kwa njia tofauti. Alijithibitisha kuwa rafiki wa kweli na mshauri mzuri, hivyo, tunapaswa kumwiga.

SIFA ZA MSHAURI MZURI

ELIHU ALIWEKA KIELELEZO KIZURI

32:4-7, 11, 12; 33:1

 

  • MWENYE SUBIRA

  • ANASIKILIZA KWA MAKINI

  • MWENYE HESHIMA

 
  • Elihu alingoja kwa subira mpaka wanaume wazee walipomaliza kuzungumza ndipo akaongea

  • Kwa sababu alisikiliza kwa makini, alikuwa na uwezo mzuri zaidi wa kuyaelewa masuala kabla ya kutoa ushauri

  • Alimwita Ayubu kwa jina na kuongea naye kama rafiki

 

33:6, 7, 32

 

  • MNYENYEKEVU

  • MWENYE KUFIKIKA

  • MWENYE HURUMA

 
  • Elihu alikuwa mnyenyekevu na mwenye fadhili, alikiri kwamba hakuwa mkamilifu

  • Alimhurumia Ayubu kwa sababu alikuwa akiteseka

 

33:24, 25; 35:2, 5

 

  • MWENYE USAWAZIKO

  • MWENYE FADHILI

  • ANAMTEGEMEA MUNGU

 
  • Elihu alimwonyesha Ayubu kwa fadhili kwamba maoni yake yalikosa usawaziko

  • Elihu alimsaidia Ayubu kuona kwamba uadilifu wa Ayubu haukuwa jambo muhimu zaidi

  • Ushauri uliofaa wa Elihu ulitayarisha njia ili Ayubu apate maagizo zaidi kutoka kwa Yehova mwenyewe