MAISHA YA MKRISTO
Vikumbusho vya Kusanyiko la Eneo
Siku zote tunataka kuongozwa na upendo kwa Mungu na jirani, kutia ndani wakati wa kusanyiko. (Mt 22:37-39) Andiko 1 Wakorintho 13:4-8 linafafanua jinsi upendo unavyoonyeshwa: “Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili. . . . Haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki. . . . Upendo haushindwi kamwe.” Unapotazama video yenye kichwa, Vikumbusho vya Kusanyiko la Eneo, fikiria njia unazoweza kuwaonyesha wengine upendo kusanyikoni.
TUNAWEZA KUONYESHAJE UPENDO . . .
-
tunapohifadhi viti?
-
kipindi cha muziki kinapokaribia kuanza?
-
mahali tunapolala?
-
kwa kujitolea?