Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Njia Mpya ya Kuanzisha Mazungumzo

Njia Mpya ya Kuanzisha Mazungumzo

Kuanzia Januari 2016, ukurasa wa nyuma wa toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi limekuwa na mfululizo wenye kichwa, “Biblia Inasema Nini?” Mfululizo huo mpya umekusudiwa kutusaidia kuanzisha mazungumzo ya habari zinazotegemea Biblia. Mfululizo huo una mpangilio unaofanana na trakti zetu. Kuna swali la maoni, jibu la Biblia, na mambo ya ziada kwa ajili ya mazungumzo.

Mara nyingi mazungumzo mazuri kuhusu habari zinazotegemea Maandiko hutusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tukitumia sehemu hiyo tutawasaidia watu wengi zaidi watosheleze njaa yao ya kiroho.—Mt 5:6.

JINSI YA KUTUMIA SEHEMU HII:

  1. Muulize mwenye nyumba maoni yake kuhusu swali moja

  2. Msikilize na umpongeze kwa jibu lake

  3. Soma andiko lililo kwenye kichwa, “Biblia Inasema Hivi,” na umwulize maoni yake kuhusu andiko hilo. Ikiwa ana muda, endeleza mazungumzo ukitumia sehemu yenye kichwa, “Ni Nini Kingine Tunachojifunza Katika Biblia?”

  4. Toa gazeti

  5. Panga kurudi ili uzungumzie swali la pili