Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

AMKENI!

Swali: Siku hizi sinema huonyesha watu wanaofanya uchawi, kuwanyonya watu damu, na mambo kama hayo. Wewe unaonaje? Hiyo ni burudani tu, au mambo hayo yana madhara?

Pendekezo: Gazeti hili la Amkeni! linaeleza sababu zinazowafanya watu wavutiwe na mambo hayo na chanzo cha mambo ya kichawi.

FUNDISHA KWELI

Swali: Ufalme wa Mungu utaondoaje matatizo ya ulimwengu huu?

Andiko: Mt 6:10

Kweli: Ufalme wa Mungu utaleta amani, umoja, na usalama duniani—kama vile ambavyo tayari umefanya mbinguni.

UFALME WA MUNGU NI NINI? (Ziara ya Kurudia)

Swali: [Zungumzia swali lililo kwenye ukurasa wa mwisho wa trakti.] Maisha yatakuwaje chini ya Ufalme wa Mungu?

Maandiko: Zb 37:29; Isa 65:21-23

Pendekezo: [Mwonyeshe broshua Habari Njema.] Somo la 7 katika broshua hii linazungumzia faida tunazoweza kupata tukiamini ahadi hizi. [Anzisha funzo la Biblia ukitumia broshua hiyo.]

ANDIKA UTANGULIZI WAKO

Ukitumia mpangilio ulioonyeshwa katika mifano iliyotangulia tayarisha utangulizi wako kwa ajili ya utumishi.