Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Unaweza Kumtia Moyo Mkristo Asiyetenda

Unaweza Kumtia Moyo Mkristo Asiyetenda

Kila mwaka, Wakristo wengi wasiotenda huhudhuria Ukumbusho. Walianza kukimbia mbio za uzima lakini wakarudi nyuma kwa sababu mbalimbali. Baadhi ya sababu hizo zimezungumziwa katika broshua Mrudie Yehova. (Ebr 12:1) Hata hivyo, wale wasiotenda bado wana thamani machoni pa Yehova, ambaye aliwanunua kwa damu ya Mwana wake. (Mdo 20:28; 1Pe 1:18, 19) Tunaweza kuwasaidiaje warudi kutanikoni?

Wazee wa kutaniko wanajitahidi kuwatafuta na kuwasaidia Wakristo wasiotenda kama tu mchungaji anavyowatafuta kwa bidii kondoo ambao wamepotea. (Lu 15:4-7) Jambo hilo linaonyesha utunzaji wenye upendo wa Yehova. (Yer 23:3, 4) Sisi sote tunaweza kuwatia moyo wasiotenda, si wazee tu. Jitihada zetu za kuonyesha fadhili na hisia-mwenzi zinampendeza Yehova na zinaweza kuwa na matokeo mazuri sana. (Met 19:17; Mdo 20:35) Kwa hiyo, fikiria ni nani unayeweza kumtia moyo, na ufanye hivyo bila kukawia!

TAZAMA VIDEO WATIE MOYO WASIOTENDA, NA KISHA UCHUNGUZE MASWALI YAFUATAYO:

  • Abbey alichukua hatua gani alipokutana na Shahidi ambaye hakumfahamu?

  • Kwa nini tunapaswa kuzungumza na wazee tunapofikiria kumsaidia mtu fulani asiyetenda?

  • Abbey alijitayarishaje ili kumtembelea Laura mara ya pili?

  • Abbey alionyeshaje uvumilivu, subira, na upendo alipokuwa akijaribu kumtia moyo Laura?

  • Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Yesu unaopatikana kwenye Luka 15:8-10?

  • Jitihada ambazo wote walifanya ili kumsaidia Laura zilitokeza baraka gani?