Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Nyimbo za Ufalme Zinatutia Moyo Tuwe na Ujasiri

Nyimbo za Ufalme Zinatutia Moyo Tuwe na Ujasiri

Paulo na Sila walimsifu Mungu kwa wimbo walipokuwa gerezani. (Mdo 16:25) Katika nyakati zetu, waamini wenzetu waliimba nyimbo za Ufalme walipokuwa katika kambi ya mateso ya Sachsenhausen nchini Ujerumani wakati wa utawala wa Wanazi na pia walipokuwa uhamishoni huko Siberia. Mifano hiyo inaonyesha jinsi nyimbo zinavyoweza kuwatia moyo Wakristo wanaokabili majaribu.

Hivi karibuni, kitabu kipya cha nyimbo chenye kichwa “Sing Out Joyfully” to Jehovah kitapatikana katika lugha nyingi zaidi. Pindi tu tutakapopata nakala zetu, tunaweza kukariri maneno yake akilini kwa kujizoeza nyimbo hizo wakati wa ibada ya familia. (Efe 5:19) Kisha, roho takatifu itatusaidia tuzikumbuke tunapopatwa na majaribu. Nyimbo za Ufalme zinaweza kutusaidia tukazie fikira tumaini letu. Zinaweza kututia moyo tunapokabili majaribu. Na hata ikiwa tuna hali nzuri, maneno yenye kuchochea ya nyimbo hizo yanatufanya ‘tuimbe kwa sauti ya kushangilia’ kwa sababu ya hali nzuri ya moyo wetu. (1Nya 15:16; Zb 33:1-3) Basi, acheni sote tutumie vizuri nyimbo zetu za Ufalme!

TAZAMA VIDEO WIMBO ULIOWATIA MOYO WAFANYAKAZI NA KISHA UJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni hali gani zilizomfanya Ndugu  Frost atunge wimbo?

  • Wimbo huo uliwatiaje moyo akina ndugu katika kambi ya mateso ya Sachsenhausen?

  • Nyimbo za Ufalme zinaweza kukutia moyo unapokuwa katika hali gani za kila siku?

  • Ni nyimbo gani za Ufalme ungependa kukariri?