Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Wakaribishe kwa Uchangamfu

Wakaribishe kwa Uchangamfu

Uwakaribishe nani kwa uchangamfu? Watu wote wanaohudhuria mikutano ya Kikristo, iwe ni mara yao ya kwanza au ni marafiki wa muda mrefu. (Ro 15:7; Ebr 13:2) Inawezekana ni mwabudu mwenzetu ambaye ametutembelea kutoka nchi nyingine au ni Mkristo asiyetenda ambaye amehudhuria mkutano kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupita. Wazia jinsi ambavyo ungehisi ikiwa ungekuwa katika hali kama yake. Je, usingethamini kusalimiwa kwa uchangamfu? (Mt 7:12) Kwa hiyo, kwa nini usijitahidi kuzunguka ndani ya Jumba la Ufalme ukiwasalimu watu kabla na baada ya mikutano? Hilo litachangia uchangamfu na upendo kutanikoni na litamtukuza Yehova. (Mt 5:16) Ni wazi kwamba huenda isiwezekane kuzungumza kibinafsi na kila mtu aliyehudhuria. Hata hivyo, kila mtu atahisi amekaribishwa kwa upendo ikiwa sisi sote tutatimiza sehemu yetu. *

Ukarimu wa kweli hauonyeshwi tu katika pindi za pekee kama vile wakati wa ukumbusho bali nyakati zote. Wageni wanapojionea upendo wa Kikristo, watachochewa kumsifu Mungu na kujiunga nasi katika ibada ya kweli.—Yoh 13:35.

^ fu. 3 Kanuni za Biblia zinatuzuia tusishirikiane na watu waliotengwa au kujitenga na ushirika ambao huenda wakahudhuria mikutano.—1Ko 5:11; 2Yo 10.