MAISHA YA MKRISTO
Utajitayarisha Jinsi Gani kwa Ajili ya Ukumbusho?
Kuanzia mwaka huu, tutakuwa na muda zaidi wa kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Siku ya Ukumbusho ikiwa katikati ya juma, Mkutano wa Huduma na Maisha hautafanywa juma hilo. Siku ya Ukumbusho ikiwa mwisho-juma, hotuba ya watu wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi halitafanywa. Je, utatumia vizuri muda huo wa ziada? Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, mipango mingi inahitaji kufanywa kwa ajili ya tukio hili la pekee. (Lu 22:7-13; km 3/15 1) Lakini mbali na mipango hiyo, sisi sote tunapaswa kutayarisha mioyo yetu. Tunaweza kufanyaje hivyo?
-
Tafakari umuhimu wa kuhudhuria.—1Ko 11:23-26
-
Chunguza uhusiano wako wa kibinafsi na Yehova na usali kuuhusu.—1Ko 11:27-29; 2Ko 13:5
-
Soma na utafakari habari za Kimaandiko kuhusu umuhimu wa Ukumbusho.—Yoh 3:16; 15:13
Wahubiri fulani husoma na kutafakari usomaji wa Biblia wa Ukumbusho ulio katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Wengine husoma mistari iliyoonyeshwa kwenye chati iliyoambatanishwa. Wengine husoma makala za Mnara wa Mlinzi zinazozungumzia Ukumbusho na upendo ambao Yehova na Yesu wametuonyesha. Hata iwe utachagua mradi gani wa kujifunza, lengo linapaswa kuwa kukusaidia umkaribie Yehova na Mwana wake hata zaidi.