Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Ni Nini Muhimu Zaidi Maishani Mwangu?

Ni Nini Muhimu Zaidi Maishani Mwangu?

Yakobo alipigana mweleka na malaika kwa ajili ya kitu muhimu sana—baraka za Yehova. (Mwa 32:24-31; Ho 12:3, 4) Namna gani sisi? Je, tuko tayari kupambana ili kumtii Yehova na kupokea baraka zake? Kwa mfano, ikiwa tunahitaji kuchagua kati ya kuhudhuria mkutano na kufanya kazi ya kimwili kwa saa kadhaa ya ziada, tutafanya uamuzi gani? Tunapompa Yehova kilicho bora, iwe ni muda wetu, nguvu zetu, au mali zetu, anatumwagia “baraka hivi kwamba [hatukosi] chochote.” (Mal 3:10) Atatuongoza, kutulinda, na kutuandalia mahitaji yetu.—Mt 6:33; Ebr 13:5.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA ENDELEA KUKAZIA FIKIRA MIRADI YA KIROHO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kitu ambacho dada huyo alipenda, kilithibitikaje kuwa jaribu?

  • Kazi yetu ya kimwili inawezaje kuwa jaribu kwetu?

  • Kwa nini Timotheo alihitaji kuendelea kujiwekea miradi hata alipokuwa mtu mkomavu kiroho?—1Ti 4:16

  • Ni nini muhimu zaidi maishani mwako?

    Ni nini kinachoonyesha kwamba kazi fulani ndiyo muhimu zaidi kwetu?