Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

“Ondoeni Kabisa Miungu ya Kigeni”

“Ondoeni Kabisa Miungu ya Kigeni”

Yakobo alijua kwamba Yehova tu ndiye anayestahili kuabudiwa, hata ingawa Yehova hakuwa ametoa sheria inayopinga ibada ya sanamu. (Kut 20:3-5) Kwa hiyo, baada ya Yehova kumwambia arudi Betheli, Yakobo alimwagiza kila mtu aliyekuwa pamoja naye aondoe kabisa miungu ya kigeni. Kisha Yakobo akatupa sanamu hizo, kutia ndani vipuli, ambavyo huenda vilivaliwa kama hirizi. (Mwa 35:1-4) Bila shaka, Yehova alipendezwa na jambo ambalo Yakobo alifanya.

Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunamwabudu Yehova peke yake? Jambo moja muhimu ni kuepuka chochote kinachohusiana na ibada ya sanamu au kuwasiliana na roho. Huenda hilo likatia ndani kuondoa vitu vyovyote vinavyohusiana na uchawi na kuchunguza burudani yetu kwa makini. Kwa mfano, jiulize: ‘Je, mimi hujiburudisha kwa kusoma vitabu au kutazama sinema zinazoonyesha vitu kama watu wanaonyonya damu, mazimwi, au mambo yanayopita uwezo wa kibinadamu? Je, burudani yangu inaonyesha kwamba mazingaombwe, uchawi, au laana ni vitumbuizo visivyo na madhara?’ Tunapaswa kuepuka kabisa kitu chochote kinachomchukiza Yehova.—Zb 97:10.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA “MPINGENI IBILISI,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni tatizo gani lililotokea katika maisha ya mwanafunzi wa Biblia anayeitwa Palesa?

  • Kwa nini ni jambo la hekima kutafuta msaada wa wazee katika visa vinavyohusisha kuwasiliana na roho?

  • Mpingeni Ibilisi, na umkaribie Mungu.​—Yak 4:7, 8

    Ikiwa tunataka kupata ulinzi wa Yehova, ni mambo gani tunayopaswa kuacha kabisa?

  • Palesa alichukua hatua gani muhimu?

  • Ni njia zipi za kuepuka uvutano wa Ibilisi katika eneo unaloishi?