MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwasaidia Watu Wenye “Mwelekeo Unaofaa” Kuwa Wanafunzi
KWA NINI NI MUHIMU: Yehova hufanya mbegu za kweli zikue katika mioyo ya wale wenye “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo 13:48; 1Ko 3:7) Tunafanya kazi pamoja naye katika huduma kwa kukazia fikira hasa wale wanaotenda kulingana na wanayojifunza. (1Ko 9:26) Wanafunzi wa Biblia wanahitaji kuelewa kwamba ubatizo wa Kikristo ni muhimu ili wapate wokovu. (1Pe 3:21) Tunawasaidia kuwa wafuasi wa Kristo kwa kuwafundisha mabadiliko wanayopaswa kufanya maishani, jinsi ya kuhubiri na kufundisha, na kujiweka wakfu kwa Yehova. —Mt 28:19, 20.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Wakumbushe wanafunzi wa Biblia kwamba kusudi la funzo lao ni kuwasaidia ‘kumjua’ Yehova na kumpendeza. —Yoh 17:3
-
Wasaidie wafanye maendeleo ya kiroho kwa kushinda vipingamizi kama vile, mazoea mabaya na marafiki wasiofaa
-
Waimarishe na kuwatia moyo kabla na baada ya ubatizo. —Mdo 14:22
TAZAMENI VIDEO YEHOVA MUNGU ATAKUSAIDIA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
Ni mambo gani yanayoweza kumfanya mtu aogope kujiweka wakfu na kubatizwa?
-
Wazee wanaweza kuwasaidiaje wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo ya kiroho?
-
Isaya 41:10 inatufundisha nini kumhusu Yehova?
-
Ni sifa zipi zitakazotusaidia kumtumikia Yehova na kupata kibali chake, hata ingawa sisi si wakamilifu?