Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwasaidia Watu Wenye “Mwelekeo Unaofaa” Kuwa Wanafunzi

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwasaidia Watu Wenye “Mwelekeo Unaofaa” Kuwa Wanafunzi

KWA NINI NI MUHIMU: Yehova hufanya mbegu za kweli zikue katika mioyo ya wale wenye “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo 13:48; 1Ko 3:7) Tunafanya kazi pamoja naye katika huduma kwa kukazia fikira hasa wale wanaotenda kulingana na wanayojifunza. (1Ko 9:26) Wanafunzi wa Biblia wanahitaji kuelewa kwamba ubatizo wa Kikristo ni muhimu ili wapate wokovu. (1Pe 3:21) Tunawasaidia kuwa wafuasi wa Kristo kwa kuwafundisha mabadiliko wanayopaswa kufanya maishani, jinsi ya kuhubiri na kufundisha, na kujiweka wakfu kwa Yehova. —Mt 28:19, 20.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Wakumbushe wanafunzi wa Biblia kwamba kusudi la funzo lao ni kuwasaidia ‘kumjua’ Yehova na kumpendeza. —Yoh 17:3

  • Wasaidie wafanye maendeleo ya kiroho kwa kushinda vipingamizi kama vile, mazoea mabaya na marafiki wasiofaa

  • Waimarishe na kuwatia moyo kabla na baada ya ubatizo. —Mdo 14:22

TAZAMENI VIDEO YEHOVA MUNGU ATAKUSAIDIA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni mambo gani yanayoweza kumfanya mtu aogope kujiweka wakfu na kubatizwa?

  • Wazee wanaweza kuwasaidiaje wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo ya kiroho?

  • Isaya 41:10 inatufundisha nini kumhusu Yehova?

  • Ni sifa zipi zitakazotusaidia kumtumikia Yehova na kupata kibali chake, hata ingawa sisi si wakamilifu?

Tunapofanya wanafunzi tunafanya kazi na Yehova jinsi gani?