Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 14-15

Alitumia Wachache Kuwalisha Wengi

Alitumia Wachache Kuwalisha Wengi

Kabla ya Pasaka ya mwaka wa 32 W.K., Yesu alifanya muujiza. Huo ndio muujiza pekee uliorekodiwa na waandikaji wote wanne wa vitabu vya Injili.

Kupitia muujiza huo, Yesu alianzisha utaratibu ambao anaendelea kuufuata hadi katika siku zetu.

14:16-21

  • Yesu aliwaelekeza wanafunzi wake walishe umati wa watu, hata ingawa walikuwa na mikate mitano na samaki wawili tu

  • Yesu alichukua mikate na samaki, na baada ya kusali akaanza kuwagawia wanafunzi wake, na wanafunzi wake wakawagawia watu

  • Chakula kiliwatosha watu wote kimuujiza, na hata kikabaki. Yesu alilisha maelfu ya watu kupitia watu wachache, yaani, wanafunzi wake

  • Yesu alitabiri kwamba katika siku za mwisho, angeandaa njia ya kutoa “chakula [cha kiroho] kwa wakati unaofaa.”—Mt 24:45

  • Mwaka wa 1919, Yesu alimweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta, wasimamie “watumishi wake wa nyumbani,” yaani, wale wanaolishwa

  • Kwa kutumia kikundi hicho kidogo cha ndugu watiwa-mafuta, Yesu anafuata utaratibu alioanzisha katika karne ya kwanza

Ninaweza kuonyeshaje kwamba ninatambua na kuheshimu njia ambayo Yesu anatumia kuwalisha watu kiroho?