Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

“Mheshimu Baba Yako na Mama Yako”

“Mheshimu Baba Yako na Mama Yako”

Yesu alipokuwa duniani, alikazia amri hii: “Mheshimu baba yako na mama yako.” (Kut 20:12; Mt 15:4) Bila shaka, Yesu alikuwa na uhuru wa kusema kwa sababu ‘aliendelea kuwatii’ wazazi wake alipokuwa kijana. (Lu 2:51) Alipokuwa mtu mzima, alihakikisha kwamba mama yake angetunzwa baada ya kifo chake. —Yoh 19:26, 27.

Katika siku zetu pia, vijana Wakristo wanaowatii wazazi wao na kuzungumza nao kwa heshima wanawaonyesha staha. Kwa kweli, amri ya kuwaheshimu wazazi inapaswa kuendelea kufuatwa milele. Hata wazazi wetu wanapozeeka, tunapaswa kuendelea kuwaheshimu na kufaidika kutokana na hekima yao. (Met 23:22) Pia, tunawaheshimu wazazi wetu waliozeeka kwa kuwatunza kihisia na kifedha inapohitajika. (1Ti 5:8) Iwe sisi ni watoto au watu wazima, kudumisha mawasiliano mazuri na wazazi wetu ni njia muhimu ya kuwaonyesha heshima.

TAZAMENI VIDEO YA VIBONZO KWENYE UBAO NINAWEZAJE KUZUNGUMZA NA WAZAZI WANGU? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini huenda ikawa vigumu kuzungumza na wazazi wako?

  • Unaweza kuwaonyeshaje wazazi wako heshima unapozungumza nao?

  • Unanufaikaje unapozungumza na wazazi wako? (Met 15:22)

    Kuzungumza na wazazi wako kunaweza kukusaidia kufanikiwa maishani