MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kutumia Maswali Vizuri
KWA NINI NI MUHIMU: Ikiwa “mawazo yaliyo moyoni mwa mtu ni kama maji yenye kina,” basi maswali ni kama ndoo inayotumiwa kuyateka. (Met 20:5) Maswali yanatusaidia kuwahusisha wasikilizaji. Majibu ya maswali yaliyoteuliwa vizuri yanatusaidia kupata habari muhimu. Yesu alitumia maswali kwa njia inayofaa. Tunaweza kumwigaje?
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Uliza maswali ya maoni. Yesu aliuliza mfululizo wa maswali ili kujua maoni ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be 238 ¶3-5) Unaweza kuuliza maswali gani ya maoni?
-
Uliza maswali ya kumsaidia mtu kufikiri. Ili kurekebisha kufikiri kwa Petro, Yesu aliuliza maswali na kumweleza mambo kadhaa ambayo yangemsaidia Petro kufikia mkataa unaofaa. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maswali gani yatakayomsaidia mtu kufikiri na kufikia mkataa unaofaa?
-
Mpongeze msikilizaji wako. Baada ya mwandishi fulani “[kujibu] kwa kutumia akili,” Yesu alimpongeza. (Mk 12:34) Unaweza kumpongeza jinsi gani mtu anayejibu swali ulilouliza?
TAZAMENI SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI AMBAYO YESU ALIFANYA—FUNDISHA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
Ingawa habari zilizozungumziwa ni sahihi, kwa nini huo ni mfano mbaya wa ufundishaji?
-
Kwa nini hatupaswi kueleza tu habari?
TAZAMENI SEHEMU YA PILI YA VIDEO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
Ndugu huyo alitumiaje maswali kwa njia yenye matokeo?
-
Ni mambo gani mengine tunayoweza kuiga kutokana na ufundishaji wake?