Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MATHAYO 12-13

Mfano wa Ngano na Magugu

Mfano wa Ngano na Magugu

Yesu alitumia mfano wa ngano na magugu kuonyesha jinsi ambavyo angekusanya jamii yote ya ngano kutoka miongoni mwa wanadamu, yaani, Wakristo watiwa-mafuta, na wakati ambapo angewakusanya; kazi ya kupanda ilianza mwaka wa 33 W.K.

13:24

‘Mtu alipanda mbegu nzuri katika shamba lake’

  • Mpandaji: Yesu Kristo

  • Mbegu nzuri inapandwa: Wanafunzi wa Yesu wanatiwa mafuta kwa roho takatifu

  • Shamba: Ulimwengu wa wanadamu

13:25

“Watu walipokuwa wamelala usingizi, adui yake akaja na kupanda magugu”

  • Adui: Ibilisi

  • Watu walipokuwa wamelala usingizi: Kifo cha mitume

13:30

“Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno”

  • Ngano: Wakristo watiwa-mafuta

  • Magugu: Wakristo wa uwongo

“Kusanyeni magugu kwanza . . . ; kisha mkusanye ngano”

  • Watumwa/wavunaji: Malaika

  • Magugu Yanakusanywa: Wakristo wa uwongo wanatenganishwa na Wakristo watiwa-mafuta

  • Kukusanya ghalani: Wakristo watiwa-mafuta wanakusanywa katika kutaniko lililorudishwa

Kipindi cha kuvuna kilipoanza, ni nini kilichowatenganisha Wakristo wa kweli na Wakristo wa uwongo?

Mimi ninanufaikaje kwa kuelewa mfano huu?