Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Endelea Kungojea kwa Hamu Huku Ukivumilia

Endelea Kungojea kwa Hamu Huku Ukivumilia

Umekuwa ukingojea Ufalme wa Mungu uje kwa muda mrefu kadiri gani? Je, umekuwa ukivumilia kwa subira licha ya hali ngumu? (Ro 8:25) Baadhi ya Wakristo wanakabili chuki, kutendewa vibaya, kufungwa gerezani, au hata hatari ya kuuawa. Wengine wengi wanakabiliana na majaribu kama vile magonjwa ya kuendelea au matatizo ya uzee.

Ni nini kitakachotusaidia kungoja kwa hamu haidhuru tunakabili jaribu gani? Tunapaswa kulisha imani yetu kila siku kwa kusoma Biblia na kutafakari. Tunahitaji kukazia fikira tumaini letu. (2Ko 4:16-18; Ebr 12:2) Ni lazima tumfikie Yehova katika sala na kumsihi atupe nguvu za roho yake takatifu. (Lu 11:10, 13; Ebr 5:7) Baba yetu mwenye upendo anaweza kutusaidia “[tuvumilie] kikamili kwa subira na shangwe.”—Kol 1:11.

TAZAMENI VIDEO LAZIMA “TUKIMBIE KWA UVUMILIVU”—UWE NA UHAKIKA KWAMBA UTAPATA TUZO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni “matukio [gani] yasiyotarajiwa” ambayo yanaweza kutupata maishani? (Mhu 9:11)

  • Sala inatusaidiaje tunapokabili majaribu?

  • Ikiwa hatuwezi kufanya mengi katika utumishi wa Yehova kama tulivyofanya zamani, kwa nini tunapaswa kukazia fikira kile ambacho bado tunaweza kufanya?

  • Kazia macho kwenye tuzo

    Ni nini ambacho hukusaidia kuwa na uhakika kwamba utapata tuzo?