Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wako Katika Huduma​—Kusitisha Mafunzo ya Biblia Yasiyo na Matokeo

Kuboresha Ustadi Wako Katika Huduma​—Kusitisha Mafunzo ya Biblia Yasiyo na Matokeo

KWA NINI NI MUHIMU: Ili watu waokolewe lazima waliitie jina la Yehova. (Ro 10:13, 14) Hata hivyo, si kila mtu anayekubali kujifunza Biblia anayetaka kuishi kupatana na viwango vya Yehova. Kwa kuwa wakati wetu ni wenye thamani sana, tunautumia vizuri katika huduma kwa kuwasaidia wale ambao kwa kweli wanataka kufanya mabadiliko ili kumpendeza Yehova. Mwanafunzi wa Biblia asipofanya maendeleo baada ya muda unaofaa kupita, ni jambo la hekima kusitisha funzo hilo na kuelekeza jitihada zetu kwa wale ambao Yehova anawavuta kwake na kwa tengenezo lake. (Yoh 6:44) Bila shaka, ikiwa wakati ujao mtu huyo ataonyesha kwamba ana “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele,” tutafurahi kuendelea kujifunza naye Biblia.—Mdo 13:48.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Mpongeze mwanafunzi kwa kutaka kupata ujuzi sahihi.—1Ti 2:4

  • Kazia umuhimu wa kutumia mambo aliyojifunza.—Lu 6:46-49

  • Kwa fadhili, zungumzia mfano wa Yesu kuhusu mpandaji, na umwombe afikirie ni nini kinachomzuia kufanya maendeleo.—Mt 13:18-23

  • Kwa busara mweleze kwa nini unasitisha funzo hilo

  • Mjulishe kwamba mara kwa mara utamtembelea ili kumtia moyo na kwamba wakati ujao funzo linaweza kuendelea ikiwa atafanya maendeleo

TAZAMENI VIDEO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Uligundua nini kutokana na mazungumzo hayo kilichoonyesha kwamba mwanafunzi hakuwa akifanya maendeleo ya kiroho?

  • Mhubiri alimsaidiaje mwanafunzi kutambua kwamba alihitaji kufanya mabadiliko?

  • Mhubiri alionyeshaje kwamba mlango bado uko wazi ili kuendeleza funzo wakati ujao?